47 Katika miaka ile saba ya shibe, mashamba ya Misri yakatoa mazao kwa wingi sana.
Mwaka ule Isaka akapanda mbegu katika inchi ile, akavuna mara mia zaidi, maana Yawe alimubariki,
Kutakuwa miaka saba ya shibe katika inchi nzima ya Misri.
Yosefu alikuwa na umri wa miaka makumi tatu alipoanza kumutumikia mufalme. Alitoka katika nyumba ya mufalme na kuitembelea inchi yote ya Misri.
Yosefu akakusanya chakula chote wakati ule wa miaka saba ya shibe na kukiweka akiba katika miji ya Misri. Katika kila muji akaweka akiba ya chakula kutoka mashamba yanayokuwa karibu na muji ule.
Inchi itoe mazao kwa wingi, vilima vijae mavuno kama ya Lebanoni, na watu wa miji wastawi kama majani.