Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 41:42 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

42 Halafu, mufalme akavua pete yake ya muhuri kwenye kidole chake na kumuvalisha Yosefu. Akamuvalisha na nguo za kitani safi na mukufu wa zahabu kwa shingo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 41:42
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yuda akamwuliza: “Unataka nikupe nini kama rehani?” Naye akamujibu: “Unipe hiyo pete na kamba yake pamoja na hiyo fimbo unayoshika.” Basi, Yuda akamupa vitu hivyo vyote, akalala naye. Tamari akapata mimba yake.


Mufalme akamupandisha katika gari lake la pili na walinzi wakatangulia mbele ya Yosefu wakilalamika kwa sauti na kusema: “Mupige magoti!” Ndivyo mufalme alivyomupa Yosefu madaraka makubwa juu ya inchi yote ya Misri.


Mordekayi, Muyuda, alikuwa wa kwanza chini ya mufalme Ahasuero katika madaraka. Alipendwa na kuheshimiwa na Wayuda, maana alitumika kwa faida na amani ya watu wake na wazao wao wote.


Mufalme akaivua pete yake, ambayo ilitumiwa kwa kupiga muhuri juu ya matangazo, akamupa adui wa Wayuda Hamani mwana wa Hamedata wa uzao wa Agagi.


Basi, siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kwanza, Hamani akawaita waandishi wote wa mufalme, akawapa tangazo ambalo alitaka litafsiriwe kwa kila luga na kila namna ya maandiko katika utawala ule, na halafu mifano ya barua isambazwe kwa watawala wote, wakubwa wa majimbo yote, na viongozi wa makabila – kufuatana na luga zinazotumika kwao. Tangazo hilo likatolewa kwa jina la mufalme Ahasuero, na kupigwa muhuri kwa pete yake.


Mordekayi alikuwa ameandika barua hizo kwa jina la mufalme Ahasuero, akazipiga muhuri kwa pete ya mufalme. Na waliozipeleka walikuwa wajumbe waliopanda juu ya farasi wenye nguvu wanaokimbia mbio.


Mordekayi alipotoka katika nyumba kwa mufalme, akiwa amevaa nguo ya kifalme ya rangi ya mayungiyungi na nyeupe, koti la kitani safi la rangi nyekundu, na taji kubwa ya zahabu, muji wa Susani ukajaa shangwe na vigelegele.


Mufalme akaivua pete yake ya muhuri aliyokuwa amemunyanganya Hamani, akamupa Mordekayi. Esteri naye akamupa Mordekayi mamlaka juu ya mali ya Hamani.


Munaweza kuwaandikia Wayuda neno lolote munalopenda. Tena munaweza kuandika kwa jina langu na kutumia muhuri wa kifalme, kwa sababu tangazo ambalo limetolewa kwa jina la mufalme na kupigwa muhuri wa mufalme, haliwezi kuvunjwa.”


Kiburi kimekuwa kama mukufu katika shingo, mateso makali ni kama nguo yao.


hayo yatakupamba kilemba cha neema juu ya kichwa chako, kama mukufu katika shingo yako.


Anajitengenezea matandiko, nguo zake ni za rangi nyeusi-nyekundu za kitani safi.


Mwanamuke huyu anatengeneza nguo na kuziuzisha, anawauzishia wachuuzi mikaba.


Pete za masikio zinapendeza mashavu yako. Mikufu ya mawe ya bei kali inapendeza shingo yako.


Umeua moyo yangu, dada yangu, muchumba wangu, umeua moyo yangu, kwa kunitupia jicho mara moja tu, na kwa ule mukufu wako katika shingo.


nguo nzuri, shemizi nzuri, vioo na vitambaa mbalimbali.


Basi, Yoyakinu alibadilisha nguo zake za wafungwa, akakuwa anapata chakula chake siku zote kwenye meza ya mufalme.


Kitani kilichopindwa vizuri kutoka Misri kilikuwa kwa kupamba tanga lako na kwa ajili ya bendera yako. Chandarua chako kilitengenezwa na nguo ya rangi ya samawi na nyekundu-nyeusi kutoka visanga vya Elisa.


Lakini, nimesikia kwamba wewe unaweza kueleza vitendawili na kutambua mafumbo. Basi, kama ukiweza kusoma maandiko haya na kunielezea maana yake, utavalishwa nguo nzuri ya rangi nyekundu na kuvalishwa mukufu wa zahabu katika shingo lako. Utapewa nafasi ya tatu katika ufalme huu.


Pale pale, mufalme Belsasari akaamuru kwamba Danieli avalishwe nguo nzuri nyekundu na mukufu wa zahabu katika shingo. Ikatangazwa kwamba Danieli atakamata sasa nafasi ya tatu katika ufalme.


Mufalme Belsasari akaamuru kwa sauti kwamba wachawi, Wakaldea wenye hekima na waaguzi waletwe. Walipoletwa, mufalme akawaambia wenye hekima hao wa Babeli: Yeyote atakayesoma maandiko haya na kunijulisha maana yake, atavalishwa nguo nzuri nyekundu za kifalme na mukufu wa zahabu katika shingo lake, na kupewa nafasi ya tatu katika ufalme.


Lakini baba yake akawaambia watumishi wake: ‘Mulete mbio kanzu nzuri sana na kumuvalisha nayo. Mumuvalishe pete kwenye kidole chake na mumuvalishe viatu.


Alivua nguo aliyovaa na kumupa Daudi pamoja na silaha zake, hata upanga, upinde na mukaba wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ