Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 41:38 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

38 Kwa hiyo mufalme akawauliza watumishi wake: “Huyu mutu ana roho wa Mungu! Tunaweza kumupata mutu mwingine kama huyu?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 41:38
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Shauri Yosefu alilotoa likaonekana kuwa jema mbele ya mufalme wa Misri na watumishi wake wote.


Nawe Ezra, kwa kutumia hekima Mungu wako aliyokupa, hiyo unayokuwa nayo, chagua wanasheria, na waamuzi watakaowaongoza wakaaji wote wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati ambao wanaishi kufuatana na Sheria ya Mungu wako. Na yule ambaye haijui Sheria hiyo, umufundishe.


Lakini ile roho inayokuwa ndani ya mutu, ile pumzi ya Mungu Mwenye Uwezo, ndiyo inayomwezesha mwanadamu kufahamu.


Mufalme anapendezwa na mutumishi anayetenda kwa hekima, lakini hasira yake inawapata wanaotenda mambo yasiyofaa.


Kuna mutu mwenye akili na maarifa ndani ya kazi? Yule atawatumikia wafalme; hatawatumikia watu wasiofaa.


Wakubwa wa muji wa Soani ni wapumbafu kabisa, washauri wa Mufalme wa Misri wanatoa shauri la kijinga! Kila mumoja anaweza namna gani kumwambia Mufalme wa Misri: Mimi ni wa uzao wa wenye hekima, wa uzao wa wafalme wa zamani!


majani yake yakiwa mazuri, na matunda yake mengi ya kukulisha viumbe vyote, nyama wa pori wakipata kivuli chini yake, na ndege wakikaa katika matawi yake,


Ee Beltesaza, unayekuwa mukubwa wa waganga, ninafahamu kuwa roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako, na kwamba hakuna fumbo linalokuwa gumu kwako. Hii ndiyo ndoto yangu; uniambie maana yake.


Katika ufalme wako kuna mutu ambaye roho ya miungu mitakatifu iko ndani yake. Wakati wa utawala wa baba yako, mutu huyu alionekana kuwa mwenye ujuzi, ufahamu na hekima kama ya miungu. Baba yako, mufalme Nebukadneza, alimufanya kuwa mukubwa wa waaguzi, wachawi, Wakaldea wenye hekima, na waganga,


Nimesikia kwamba roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako, na kwamba una ujuzi, na akili, na hekima ya ajabu.


Aliweka vilevile wakubwa watatu, Danieli akiwa mumoja kati yao, wawasimamie wale wakubwa wengine katika uongozi kusudi mufalme asipatwe na hasara.


Danieli akaonekana kuwa bora kuliko wale wasimamizi wengine na wakubwa wote kwa maana alikuwa na roho njema. Hivyo mufalme akakusudia kumupa uongozi wa ufalme wote.


Yawe akamwambia Musa: Umutwae Yoshua mwana wa Nuni, mutu mwenye roho nzuri, kisha uweke mikono juu yake,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ