Nawe Ezra, kwa kutumia hekima Mungu wako aliyokupa, hiyo unayokuwa nayo, chagua wanasheria, na waamuzi watakaowaongoza wakaaji wote wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati ambao wanaishi kufuatana na Sheria ya Mungu wako. Na yule ambaye haijui Sheria hiyo, umufundishe.
Wakubwa wa muji wa Soani ni wapumbafu kabisa, washauri wa Mufalme wa Misri wanatoa shauri la kijinga! Kila mumoja anaweza namna gani kumwambia Mufalme wa Misri: Mimi ni wa uzao wa wenye hekima, wa uzao wa wafalme wa zamani!
majani yake yakiwa mazuri, na matunda yake mengi ya kukulisha viumbe vyote, nyama wa pori wakipata kivuli chini yake, na ndege wakikaa katika matawi yake,
Ee Beltesaza, unayekuwa mukubwa wa waganga, ninafahamu kuwa roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako, na kwamba hakuna fumbo linalokuwa gumu kwako. Hii ndiyo ndoto yangu; uniambie maana yake.
Katika ufalme wako kuna mutu ambaye roho ya miungu mitakatifu iko ndani yake. Wakati wa utawala wa baba yako, mutu huyu alionekana kuwa mwenye ujuzi, ufahamu na hekima kama ya miungu. Baba yako, mufalme Nebukadneza, alimufanya kuwa mukubwa wa waaguzi, wachawi, Wakaldea wenye hekima, na waganga,
Danieli akaonekana kuwa bora kuliko wale wasimamizi wengine na wakubwa wote kwa maana alikuwa na roho njema. Hivyo mufalme akakusudia kumupa uongozi wa ufalme wote.