Lakini hata nyuma ya kuwakula wale wanono, mutu yeyote asingeweza kutambua kwamba wamewakula wenzao, maana walikuwa tu wamekonda sana kama vile mwanzo. Halafu nikaamuka katika usingizi.
Wale ngombe saba waliokonda sana, ambao waliwafuata wale wanono, na yale masuke matupu saba, yaliyokaushwa na upepo mukali wa jangwa, maana yake ni miaka saba ya njaa.
Ikaanza miaka saba ya njaa kama vile Yosefu alivyokuwa amesema pale mbele. Inchi zingine zote zikakuwa na njaa, lakini inchi yote ya Misri ilikuwa na chakula.
Halafu, Gadi akamwendea Daudi na kumwelezea, akisema: “Unapendelea njaa ya miaka saba ikuje katika inchi yako? Au wewe uwakimbie waadui zako kwa miezi mitatu wanapokufuatilia? Au kuwe siku tatu ambapo inchi yako itakuwa na ugonjwa mukali? Fikiri unipe jibu nitakalomupa yeye aliyenituma.”
Basi Elia wa kijiji cha Tisibe katika jimbo la Gileadi akamwambia mufalme Ahabu: “Kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye ninamutumikia, anavyoishi, hakutakuwa umande wala mvua mpaka nitakapotoa amri.”
Elisha alikuwa amemwambia mwanamuke aliyeishi Sunemu ambaye alikuwa amemufufua mwana wake: “Ondoka na jamaa yako, uhamie katika inchi ya kigeni kwa sababu Yawe ameleta njaa itakayokuwa katika inchi kwa muda wa miaka saba.”
Basi, mwenye kujitakia baraka katika inchi, atajitakia baraka kwa Mungu wa kweli. Mwenye kuapa katika inchi hii, ataapa kwa Mungu wa kweli. Maana taabu za zamani zimepita zimetoweka kabisa mbele yangu.
Ninawaambia ukweli: kulikuwa wajane wengi katika inchi ya Israeli katika siku za nabii Elia. Wakati ule, mvua ilifungwa isinyeshe kwa muda wa miaka mitatu na nusu na kukakuwa njaa kubwa katika inchi yote.