Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 41:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Halafu Yosefu akamwambia mufalme: “Ndoto zako zote mbili zina maana moja tu. Mungu amekufunulia mambo atakayofanya sasa hivi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 41:25
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakamujibu: “Tuna huzuni kwa sababu tumeota ndoto na hakuna anayeweza kututafsiria ndoto zetu.” Yosefu akawaambia: “Kutafsiri ndoto si kazi ya Mungu? Basi, muniambie ndoto zenu.”


Yosefu akamujibu: “Sina uwezo ule; lakini Mungu atakupa jibu linalofaa.”


Ngombe wale saba wazuri ni miaka saba, na yale masuke saba mazuri vilevile ni miaka saba. Ndoto hiyo tafsiri yake ni moja.


Kama vile nilivyokuelezea, ee mufalme, Mungu amekufunulia mambo atakayofanya sasa hivi.


Ndoto yako ilirudiliwa mara mbili kwa mifano inayofanana kwa kukuonyesha kwamba Mungu ameamua, naye atatimiza jambo hili sasa hivi.


Yawe ameonyesha ushindi wake; ameonyesha wazi kwa mataifa uwezo wake wa kuokoa.


Maana mara hii, wewe mwenyewe, wakubwa wako na watu wako mutapatwa na mapigo yangu makali. Nawe utatambua kwamba hakuna yeyote katika dunia anayekuwa kama mimi.


Mataifa yote yakusanyike, watu wote wakutane pamoja. Nani kati ya miungu yao anayeweza kutangaza yatakayotukia? Nani anayeweza kutuonyesha yanayotukia sasa? Wawalete washuhuda wao, kuhakikisha kwamba walifanya hivyo. Uwaache wasikilize na kusema: Ilikuwa kweli.


Uliliona jiwe lililoongoka lenyewe toka kwenye mulima, bila kuguswa, na jinsi lilivyoivunja vipandevipande ile sanamu iliyotengenezwa kwa chuma, shaba, udongo wa mufinyanzi, feza na zahabu. Ee mufalme, Mungu Mukubwa amekufunulia mambo yatakayotukia nyuma. Ni mimi ninayekuelezea hivyo. Ndoto yako ni ya kweli na maana yake ni ya kuaminiwa.


Mufalme akamwambia Danieli: Hakika, Mungu wako ni Mungu wa miungu na Bwana wa wafalme, na ndiye anayefumbua mafumbo kwa sababu ameweza kunifumbulia fumbo hili.


Hakika, Bwana wetu Yawe hafanyi kitu bila kuwafunulia watumishi wake manabii nia yake.


Wakati ule, watu wawili watakutiwa katika shamba moja; mumoja atapelekwa na mwingine ataachwa.


Lakini ninyi mujiangalie vizuri, kwa maana nimewaambia hayo yote mbele.


Ninamwomba Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba mwenye utukufu, awapatie Roho wake kusudi mukuwe na hekima na ufunuo hata muweze kumujua.


Yawe akamwambia Yoshua: “Usiwaogope hao, maana kesho, wakati kama huu, nitawaangamiza wote kwa kuwatia katika mikono ya Waisraeli; nanyi mutakata mishipa ya miguu ya farasi wao na kuteketeza magari yao kwa moto.”


Nyuma ya mambo hayo nilipata maono mengine. Niliona mulango mumoja umefunguliwa wazi mbinguni. Halafu ile sauti niliyosikia mara ya kwanza, iliyolia kama baragumu, ikaniambia: “Panda huku, nami nitakuonyesha mambo yanayopaswa kutokea nyuma ya hayo ya mbele.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ