19 Hao wakafuatwa na ngombe wengine saba zaifu, wembamba na wamekonda sana. Mimi sijapata kuona ngombe wa hali hiyo katika inchi ya Misri.
nikaona ngombe saba wazuri na wanono wakitoka katika muto na kula nyasi.
Basi, wale ngombe waliokonda sana wakakula wale ngombe saba wanono.
Halafu, nyuma ya wale, ngombe wengine saba waliokonda sana wakatoka katika muto Nili, wakakuja na kusimama karibu na wale ngombe wazuri na wanono, kando ya muto.
“Musitoe sadaka kwa Yawe, Mungu wenu, ngombe au kondoo mwenye kilema; hiyo ni chukizo kwa Yawe, Mungu wenu.