Baba yake akamwambia: “Kwenda uwaangalie wandugu zako na nyama kama wako salama, kisha uniletee habari.” Basi, Yakobo akamutuma Yosefu kutoka bonde la Hebroni. Yosefu alipokaribia Sekemu,
Wakamujibu: “Tuna huzuni kwa sababu tumeota ndoto na hakuna anayeweza kututafsiria ndoto zetu.” Yosefu akawaambia: “Kutafsiri ndoto si kazi ya Mungu? Basi, muniambie ndoto zenu.”
Mufalme akamwambia: “Yawe asipokusaidia, mimi nitaweza kukupa musaada kutoka wapi? Kutoka katika kiwanja cha kupepetea ngano au kutoka katika kikamulio?
Mufalme akamwambia Danieli: Hakika, Mungu wako ni Mungu wa miungu na Bwana wa wafalme, na ndiye anayefumbua mafumbo kwa sababu ameweza kunifumbulia fumbo hili.
Yule malaika akaniambia vilevile niseme neno hili la Yawe juu ya Zerubabeli: Hauwezi kushinda kwa nguvu au kwa uwezo wako mwenyewe, lakini kwa musaada wa roho wangu. –Ni Yawe wa majeshi anayesema.
Petro alipoona maneno yale, akawaambia watu: “Wanainchi wenzangu Waisraeli, sababu gani munashangazwa na jambo hili? Sababu gani munatukazia macho? Munafikiri kwamba mutu huyu amepata kutembea kutokana na uwezo wetu sisi wenyewe au kwa haki yetu mbele ya Mungu?
Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa sawa hivi ninavyokuwa, na neema yake niliyopewa haikukuwa ya bure, lakini nilitumika zaidi sana kuliko mitume wote wengine. Hakika si mimi, lakini ni neema ya Mungu inayokuwa pamoja nami.