Akaota ndoto, na katika ndoto hiyo, aliona ngazi iliyosimamishwa juu ya dunia na incha yake inafika mbinguni. Wamalaika wa Mungu walikuwa wakipanda na kushuka katika ngazi hiyo.
Basi, usiku mumoja, yule mutunza vinywaji mukubwa na yule mupishi mukubwa wa mukate wa mufalme, waliota ndoto mule ndani ya gereza, kila mumoja na ndoto yake tofauti.
Kisha mufalme wa Misri akawaamuru watu wake wote hivi: “Kila mutoto mwanaume atakayezaliwa kwa Waebrania mumutupe ndani ya muto Nili. Lakini kila mutoto mwanamuke, mumwache aishi.”
Lakini wasipoamini hata vitambulisho hivi viwili, au kuamini maneno yako, utachota maji ya muto Nili na kuyamwanga juu ya inchi kavu. Maji hayo yatakuwa damu juu ya inchi kavu.”
Umwambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi nitapingana na wewe mufalme wa Misri, wewe mamba unayelala ndani ya muto Nili! Wewe unafikiri kwamba muto Nili ni wako, kwamba wewe ndiwe uliyeufanya!
Kwa sababu umesema kwamba muto Nili ni wako, kwamba ndiwe uliyeufanya, basi, inchi yako, Misri, itakuwa tupu na jangwa. Halafu watu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
Pilato alipokuwa amekwisha kuikaa kwa kuamua maneno, muke wake akamutumia ujumbe huu: “Usijiingize katika maneno ya mutu huyo mwenye haki, kwa sababu usiku niliteseka sana katika ndoto kwa ajili yake.”
Inchi munayokwenda kurizi si kama inchi ya Misri mulikotoka, ambako mulipanda ngano nanyi mulipaswa kuleta maji kutoka kwenye mito kwa kuimwangilia kama vile mulivyofanya kwa mashamba ya mboga.