Mwanzo 40:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
5 Basi, usiku mumoja, yule mutunza vinywaji mukubwa na yule mupishi mukubwa wa mukate wa mufalme, waliota ndoto mule ndani ya gereza, kila mumoja na ndoto yake tofauti.
Wakati fulani nyuma ya mambo hayo, wakubwa wawili waliomutumikia mufalme wa Misri wakamukosea. Wakubwa wale walikuwa mutunza vinywaji mukubwa na mupishi mukubwa wa mukate wa mufalme.
Wakamujibu: “Tuna huzuni kwa sababu tumeota ndoto na hakuna anayeweza kututafsiria ndoto zetu.” Yosefu akawaambia: “Kutafsiri ndoto si kazi ya Mungu? Basi, muniambie ndoto zenu.”
Kisha, Danieli akafika, anayeitwa vilevile Beltesaza, jina la mungu wangu, ambaye roho ya miungu mitakatifu iko ndani yake, nami nikamwelezea ndoto yangu, nikasema:
Majani yake yalikuwa mazuri. Ulikuwa umejaa matunda mengi yaliyotoshelea kwa kulisha dunia nzima. Nyama wote wa pori walipata kivuli chini yake, na ndege wa anga walikaa katika matawi yake. Viumbe vyote vilipata chakula kutoka muti huo.