Basi, Yosefu aliposhushwa kwenda mpaka Misri, Mumisri mumoja anayeitwa Potifari ambaye alikuwa jemadari wa mufalme wa Misri na mukubwa wa waaskari walinzi, akamununua kutoka kwa Waisimaeli waliomuleta Misri.
Hivyo mukubwa wa kifungo akamuweka Yosefu akuwe mukubwa wa wafungwa wote mule katika kifungo. Kila kitu kilichofanyika mule kilifanywa kwa mamlaka yake.
Yule mukubwa wa kifungo hakujishugulisha tena na kitu chochote Yosefu alichopewa kwa maana Yawe alikuwa pamoja na Yosefu na kufanikisha kila kitu alichofanya.