Nyuma ya siku tatu mufalme atakunyanyua kutoka katika kifungo na kukurudisha tena katika cheo chako. Utaweza tena kumupa mufalme kikombe kwa mukono kama ulivyokuwa unafanya pale mbele.
Ee Bwana, usikilize maombi yangu mimi mutumishi wako na ya watumishi wako wanaofurahia kukutii wewe. Ninakuomba unifanikishe leo, mimi mutumishi wako, na kunijalia kuhurumiwa na mufalme.” Mimi nilikuwa na madaraka ya kumupa mufalme kinywaji.
Katika mwezi wa Nisani, kwa mwaka wa makumi mbili wa utawala wa mufalme Artasasta, wakati divai ilipokuwa mbele yake, nilitwaa divai na kumupatia mufalme. Mpaka sasa nilikuwa sijapata kuwa na huzuni mbele yake.