Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 40:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Ilipotimia siku ya tatu, ambayo ilikuwa siku ya kufanya sikukuu ya kuzaliwa kwake, mufalme wa Misri akafanyia watumishi wake wote karamu. Akatoa katika kifungo mutunza vinywaji wake mukubwa na mupishi mukubwa wa mikate, akawaweka mbele ya wakubwa wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 40:20
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Isaka akaendelea kukomaa, na siku alipoachishwa kunyonya, Abrahamu akafanya karamu kubwa.


Nyuma ya siku tatu mufalme atakunyanyua kutoka katika kifungo na kukurudisha tena katika cheo chako. Utaweza tena kumupa mufalme kikombe kwa mukono kama ulivyokuwa unafanya pale mbele.


Nyuma ya siku tatu mufalme atakunyanyua kutoka katika kifungo, atainua kichwa chako kusudi akutundike juu ya muti, nao ndege watakula mwili wako.”


Solomono alipoamuka, alitambua kwamba ilikuwa ndoto. Halafu akarudi Yerusalema, akasimama mbele ya Sanduku la Agano la Yawe, akamutolea sadaka za kuteketezwa na za amani. Halafu akawafanyia watumishi wake wote karamu.


Katika mwaka wa makumi tatu na mbili, Ewili-Merodaki mufalme wa Babeli alianza kutawala. Mwaka uleule akamusamehe Yoyakini mufalme wa Yuda, akamufungua. Hayo yalitokea katika siku ya makumi mbili na saba ya mwezi wa kumi na mbili wa mwaka wa makumi tatu na saba tangu Yoyakini alipopelekwa katika uhamisho.


Katika mwaka wa tatu wa utawala wake, mufalme Ahasuero akaandaa karamu kwa ajili ya viongozi na watumishi wake wa serikali, wakubwa wa majeshi ya Persia na Media, watu wenye heshima na wakubwa wa majimbo.


Kisha hayo, Yobu akaamua kusema. Akalaani siku aliyozaliwa.


mpaka kile alichotabiri kilipotimia. Neno la Yawe likahakikisha kwamba alikuwa na haki.


Katika mwaka wa makumi tatu na saba tangu Yoyakinu mufalme wa Yuda alipopelekwa katika uhamisho, siku ya makumi mbili na tano ya mwezi wa kumi na mbili, Ewili-Merodaki akakuwa mufalme wa Babeli. Mwaka uleule alipofanywa mufalme, alimusamehe Yoyakinu mufalme wa Yuda, akamwondoa katika kifungo.


Na ilikuwa kwa sikukuu ya kuzaliwa kwa Herode, binti ya Herodia akacheza mbele ya wote walioalikwa. Binti yule akamupendeza Herode sana


“Kulipopita siku nyingi, bwana wa watumishi wale akarudi, akafanya hesabu ya mali yake pamoja nao.


Siku moja Herodia alipata wakati wa kumwua Yoane. Ilikuwa sikukuu ya kuzaliwa kwa Herode, wakati alipofanya karamu kwa wasimamizi wa serikali yake, wakubwa wa waaskari na waheshimiwa wa Galilaya.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ