Nyuma ya siku tatu mufalme atakunyanyua kutoka katika kifungo na kukurudisha tena katika cheo chako. Utaweza tena kumupa mufalme kikombe kwa mukono kama ulivyokuwa unafanya pale mbele.
Katika kitunga cha juu, kulikuwa aina mbalimbali za mikate kwa ajili ya mufalme. Lakini, ndege walikuwa wakikula kutoka kitunga kile juu ya kichwa changu!”
Ilipotimia siku ya tatu, ambayo ilikuwa siku ya kufanya sikukuu ya kuzaliwa kwake, mufalme wa Misri akafanyia watumishi wake wote karamu. Akatoa katika kifungo mutunza vinywaji wake mukubwa na mupishi mukubwa wa mikate, akawaweka mbele ya wakubwa wake.
Kisha, Risipa binti ya Aya alitwaa nguo ya gunia, akajitandikia juu ya jiwe kubwa. Alikaa pale tangu mwanzo wa mavuno mpaka wakati wa mvua ulipofika na kuinyeshea maiti. Wakati huo wote, aliwafukuza ndege na wanyama wa pori, usiku na muchana, kusudi wasifikie maiti hizo.
Basi, utupatie watu saba kati ya wazao wake, nasi tuwatundike mbele ya Yawe juu ya mulima Gibea, kwa Saulo aliyechaguliwa na Yawe.” Mufalme akasema: “Nitawapatia nao.”
Utakufa juu ya milima ya Israeli, wewe pamoja na makundi yako yote ya waaskari na mataifa yanayokuwa pamoja nawe. Nami nitaitoa miili yao ikuliwe na ndege wa kila aina na nyama wakali.
Kristo alitukomboa toka laana ya Sheria, akijitwalia laana hiyo kwa ajili yetu. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mutu yeyote anayetundikwa juu ya muti amelaaniwa.”
Kisha akamutundika mufalme wa Ai juu ya muti wa tini mpaka magaribi. Lakini jua lilipoanza kutua, Yoshua aliamuru maiti yake iondolewe juu ya muti na kutupwa kwenye mulango wa muji kisha walundike lundo kubwa la mawe juu ya maiti hiyo. Lundo hilo liko kule mpaka leo.
Siku ya leo, Yawe atakutia katika mikono yangu. Nitakushinda, nitakukata kichwa chako; na miili ya waaskari wa Wafilistini nitawapa ndege na nyama wa pori. Halafu dunia nzima itajua kwamba Mungu yuko katika Israeli.