6 Yawe akamwambia Kaina: “Kwa nini umekasirika, na kwa nini uso wako umekunjamana?
Ukitenda vyema hautakubaliwa? Na usipotenda vyema, basi, zambi inajificha kwa mulango; inakutamani, lakini unapaswa kuishinda.”
Kweli mahangaiko yanamwua mupumbafu, na wivu unamwangamiza mujinga.
Yawe anasema hivi: Mukuje basi, tukate shauri. Zambi zenu zikionekana kuwa nyekundu, zitakuwa nyeupe kama teluji; zikionekana kuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama sufu.
Enyi watu! Musikilize vile mimi Yawe ninavyosema: Nimekuwa kama vile jangwa au inchi yenye giza kubwa? Kwa nini basi watu wangu wanasema: Sisi tuko watu huru; hatutakurudilia!
Yawe anasema hivi: Babu zenu waliona kosa gani kwangu hata wakanigeuka na kuniacha, wakakimbilia miungu ya bure, hata nao wakakuwa watu bure?
Naye Yawe akamujibu Yona: Unazani kwamba unafanya vema kukasirika?
Lakini Mungu akamwuliza Yona: Unazani unafanya vema kuukasirikia mumea huo? Yona akajibu: Ndiyo, ninafanya vema kukasirika – kukasirika hata kufa!
Sina haki ya kutumia mali yangu sawa ninavyotaka? Unapatwa na wivu kwa sababu mimi ni mwema?’ ”