Ubaguzi wao unashuhudia juu yao; wanatangaza zambi yao kama vile watu wa Sodoma, wala hawaifichi. Ole kwao watu hao, kwa sababu wamejiletea maangamizi wenyewe.
Kwa njia ya imani, Abeli alimutolea Mungu sadaka nzuri zaidi kuliko ile ya Kaina. Kwa ajili ya imani yake alihesabiwa na Mungu kuwa mwenye haki, kwa maana Mungu mwenyewe alikubali sadaka zake. Na kwa imani ile, ingawa Abeli amekwisha kufa, angali anasema.
Ole kwao! Maana wamefuata njia ya Kaina. Kwa ajili ya kupata mali wameanguka katika kosa Balama alilofanya. Wameangamia kwa sababu wameasi kama vile Kora alivyoasi.
Lakini Yawe alimwambia: “Usiangalie sura yake wala urefu wake. Mimi nimemukataa maana siangalii mambo kama vile wanadamu wenye kufa wanavyoangalia. Mwanadamu anaangalia umbo la inje, lakini mimi ninaangalia ndani ya moyo.”