Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 4:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 naye Abeli akamutolea Mungu sadaka ya wazao wa kwanza wa kondoo wake na nyama nono. Yawe akapendezwa na Abeli pamoja na sadaka yake,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 4:4
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Jua lilipokwisha kutua na giza kuingia, furu inayofuka moshi na mwenge unaowaka moto vikapita katikati ya vile vipande vya nyama.


Nyuma ya muda fulani, Kaina akamutolea Yawe sadaka kutoka mazao ya shamba,


Kisha, wao watamwomba mungu wao, nami nitamwomba Yawe. Mungu atakayejibu kwa kuleta moto, yule ndiye Mungu wa kweli.” Na pale watu wote wakasema: “Sawa!”


Mara moja, Yawe akashusha moto, ukaiteketeza sadaka ile ya kuteketezwa, kuni, mawe na mavumbi, na kuyakausha maji yote katika mufereji.


Kisha Daudi akamujengea Yawe mazabahu pahali pale na kumutolea sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani. Akamwomba Yawe, naye akakubali maombi yake kwa kuleta moto kutoka mbinguni na kuteketeza sadaka kwenye mazabahu.


Solomono alipomaliza maombi yake, moto ukashuka kutoka mbinguni na kuchoma sadaka na sadaka za kuteketeza kwa moto zilizotolewa, kisha utukufu wa Yawe ukajaza nyumba.


Akupelekee musaada kutoka katika hekalu lake; akukinge tokea kwenye mulima Sayuni.


munapaswa kumuwekea Yawe kila muzaliwa wenu wa kwanza mwanaume. Kila muzaliwa wa kwanza dume wa mifugo yenu atakuwa wa Yawe.


Umuheshimu Yawe kwa mali yako, na kwa malimbuko ya mazao yako yote.


Tena nilitambua kwamba mutu anatoa jasho na kutumia ujuzi wake juu ya wivu tu kwa mwenzake. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Yawe akawasha moto ukaiteketeza sadaka ya kuteketezwa na mafuta yaliyokuwa juu ya mazabahu. Watu wote walipoona huo moto wakapiga vigelegele na kuinama uso mpaka chini.


Musa akakasirika sana, akamwambia Yawe: Usikubali sadaka za watu hawa. Mimi sijatwaa punda wa mutu yeyote, wala sijamuzuru mutu!


Kisha Yawe akashusha moto ukawateketeza wale watu mia mbili makumi tano waliokwenda kufukiza ubani.


Ninakupa vitu vyote vizuri vinavyotokana na malimbuko ambayo Waisraeli wananitolea: mafuta safi, divai na ngano.


Lakini wazaliwa wa kwanza wa ngombe, kondoo au mbuzi wasikombolewe; hao ni watakatifu. Damu yao utainyunyizia mazabahu na mafuta yao utayateketeza kuwa sadaka ya kuteketezwa ambayo ni harufu nzuri inayonipendeza mimi Yawe.


Kwa njia ya imani, Abeli alimutolea Mungu sadaka nzuri zaidi kuliko ile ya Kaina. Kwa ajili ya imani yake alihesabiwa na Mungu kuwa mwenye haki, kwa maana Mungu mwenyewe alikubali sadaka zake. Na kwa imani ile, ingawa Abeli amekwisha kufa, angali anasema.


Na kufuatana na Sheria, karibu vitu vyote vinatakaswa kwa damu, nazo zambi haziwezi kusamehewa pasipo kumwangwa kwa damu.


Wakaaji wote wa dunia watamwabudu, ndio wale wote ambao tangia kuumbwa kwa dunia, majina yao hayakuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa.


Malaika wa Yawe akanyoosha fimbo yake, akagusa nyama na mikate kwa incha ya fimbo. Kwa rafla, moto ukatoka ndani ya jiwe, ukateketeza nyama na mikate. Mara moja malaika wa Yawe akatoweka mbele yake.


Halafu Samweli akamwambia: “Unazani kwamba Yawe anapendelea zaidi sadaka za kuteketezwa kwa moto na matoleo mengine, kuliko kuitii sauti yake? Hapana. Kumutii yeye ni bora kuliko matoleo na kumusikiliza kuliko kumutolea mafuta ya beberu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ