Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 4:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Kisha Kaina akaondoka mbele ya Yawe, akaenda kuishi katika inchi ya Nodi, upande wa mashariki wa Edeni.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 4:16
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Magaribi mwanaume na muke wake wakasikia Yawe Mungu akitembea katika bustani, nao wakajificha kati ya miti ya bustani, Yawe Mungu asipate kuwaona.


Angalia, leo umenifukuza kutoka udongo wenye mboleo na mbali nawe. Basi, nitakuwa mukimbizi na mwenye kutangatanga katika dunia, na yeyote atakayeniona ataniua.”


Kaina akalala na muke wake, naye muke wake akapata mimba, akazaa Enoki. Kaina akajenga muji akauita kwa jina la mwana wake Enoki.


Lakini Yawe aliwarehemu na kuwaonea huruma. Aliwaangalia kwa wema kwa sababu ya agano lake na Abrahamu, Isaka na Yakobo. Hakuwaangamiza wala hajawaachilia hata kidogo mpaka leo.


Yawe aliwakasirikia sana watu wa Yerusalema na Yuda, hata akawafukuza mbali naye. Zedekia alimwasi mufalme wa Babeli.


Yawe akamwambia Shetani: “Basi, unaweza kufanya vile unavyotaka juu ya mali yake. Lakini tu yeye mwenyewe usimuguse.” Basi, Shetani akaondoka mbele ya Yawe.


Kwa hiyo Shetani akaondoka mbele ya Yawe, akamutesa Yobu kwa vidonda vikali tangia kwenye miguu yake mpaka kwenye kichwa chake.


Hataona tena mitiririko ya asali na ya maziwa.


Ee Mungu, uwaazibu kwa makosa yao, waanguke katika mipango yao wenyewe; uwafukuze inje kwa sababu ya zambi zao nyingi, kwa sababu wamekuasi wewe.


Mungu asimame sasa, na waadui zake watawanyike! Wanaomuchukia wakimbie mbali naye!


Watu waliposikia ngurumo na kuona umeme ukiwaka na kusikia sauti ya baragumu juu ya mulima uliokuwa unafuka moshi, wote wakaogopa na kutetemeka. Wote wakasimama mbali,


mimi nitawanyanyua na kuwatupilia mbali, wao wenyewe pamoja na muji niliowapa wao na babu zao.


Yawe aliwakasirikia sana watu wa Yerusalema na Yuda hata akawafukuza mbali naye. Zedekia alimwasi mufalme wa Babeli.


Basi, Yona akasimama kwa kukimbilia Tarsisi, mbali na uso wa Yawe. Akaenda mpaka katika muji wa Yofa ambapo alikuta mashua moja iko tayari kwenda Tarsisi. Alilipa bei ya safari, akapanda ndani ya mashua, akasafiri pamoja na watu wengine kwenda Tarsisi, mbali na uso wa Yawe.


Kwa maana pahali popote watu wawili au watatu wanapokusanyika kwa ajili ya jina langu, mimi ni pale katikati yao.”


Halafu mutaanza kumwambia: ‘Sisi tulikula na kunywa pamoja nawe, na wewe ulifundisha katika barabara za muji wetu.’


Neno alikuwa yuko katika dunia, nayo dunia iliumbwa kwa njia yake, lakini ijapokuwa vile haikumutambua.


Vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, wala hakuna hata kitu kimoja kilichoumbwa pasipo yeye.


Wao wenyewe wanaeleza namna mulivyotupokea wakati tulipofika kwenu na namna mulivyoacha kuabudu sanamu na kumurudilia Mungu. Mulifanya vile kusudi mumutumikie Mungu mwenye uzima na wa kweli


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ