Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 4:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Angalia, leo umenifukuza kutoka udongo wenye mboleo na mbali nawe. Basi, nitakuwa mukimbizi na mwenye kutangatanga katika dunia, na yeyote atakayeniona ataniua.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 4:14
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alimufukuza inje. Akaweka makerubi upande wa mashariki wa bustani ya Edeni wakiwa na upanga wa moto uliogeuka huku na kule, kwa kulinda njia inayokwenda kwenye muti wa uzima.


Kaina akamwambia Yawe: “Azabu yangu ni kubwa sana. Siwezi kuivumilia.


Sasa wandugu zangu wote wamenigeuka mimi mujakazi wako. Wanataka nimutoe katika mikono yao yule mutoto aliyemwua mwenzake kusudi wamwue kwa kuyaangamiza maisha ya ndugu yake. Hivyo, watamwua huyu ambaye sasa ndiye murizi. Wakifanya hivyo, watazimisha kabisa tumaini langu lililobakia, na mume wangu hataachiwa jina wala muzao katika dunia.”


Watoto wake watangetange na kuombaomba; wafukuzwe katika mabaki ya nyumba zao!


Kusikuwe mutu wa kumutendea mema, au kuwatunza watoto wake wayatima!


Ee Yawe, unijibu haraka; maana roho yangu imeregea kabisa! Usinigeuzie mugongo, kusudi nisikuwe kama wale wanaoshuka katika shimo la wafu.


Mwovu anaangamizwa kwa matendo yake maovu, lakini mwenye haki atapata usalama kwa uaminifu wake.


Waovu wanakimbia ijapokuwa hawafukuzwi na mutu, lakini wenye haki ni hodari kama simba.


na kuiangalia dunia, lakini wataona tu taabu, giza na mateso makubwa. Hakuna atakayeepuka giza hilo kubwa.


Yawe aliwakasirikia sana watu wa Yerusalema na Yuda hata akawafukuza mbali naye. Zedekia alimwasi mufalme wa Babeli.


Basi, watatoweka kama ukungu wa asubui, kama umande unaotoweka upesi; kama makapi yanayopeperushwa kwenye nafasi ya kupepetea, kama moshi unaotoka katika munara wa kutoshea moshi inje.


Mimi nitawashambulia, nanyi mutapigwa na waadui zenu. Mutatawaliwa na wale wanaowachukia. Mutatishwa na kukimbia hata kama hakuna mutu yeyote anayewafukuza.


Na kwa njia ya wamoja wenu watakaobaki nitaleta woga ndani ya moyo wao, katika inchi ya waadui zao hata jani linalopeperushwa litawakimbiza. Watakimbia kama mutu anayekimbia vita. Watakimbia na kuanguka hata kama hakuna mutu anayewafukuza.


Ndugu wa karibu wa mutu aliyeuawa atalipiza kisasi. Huyu atakapokutana na huyo mwuaji, atatimiza hukumu ya kifo.


au kwa kumupiga ngumi akikufa, basi mutu huyo aliyemupiga mwenzake ni mwuaji na anapaswa kuuawa. Ndugu wa karibu wa mutu aliyeuawa atalipiza kisasi atakapokutana naye.


halafu ndugu ya mutu aliyeuawa akimukuta inje ya mipaka ya muji huo wa makimbilio akimwua, huyo hatakuwa na kosa la kuua.


“Kisha mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kushoto: ‘Muondoke hapa karibu nami, ninyi muliolaaniwa! Muende katika moto usiozimika hata milele, uliotayarishwa kwa ajili ya Shetani na wamalaika wake!


Halafu hawa watakwenda kwenye nafasi watakapoazibiwa kwa milele, lakini wenye haki wataingia kwenye uzima wa milele.”


Yawe atawatawanya kati ya mataifa yote, kutoka pembe moja ya dunia mpaka nyingine na huko mutaitumikia miungu mingine ya miti na mawe, miungu ambayo ninyi wala wazee wenu hamukuijua.


Hamutakuwa na raha yoyote pahali penu wenyewe pa kutulia wala kati ya mataifa hayo. Lakini Yawe atawapa huko wasiwasi wa moyo, kufifia kwa macho na mahangaiko ya ndani ya roho.


Azabu yao itakuwa kuangamizwa kwa milele, na kutengwa mbali na uso wa Bwana na mbali na utukufu wa uwezo wake,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ