Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 4:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Yawe akasema: “Umefanya nini? Damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika udongo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 4:10
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Yawe akasema: “Kuna malalamiko mengi juu ya watu wa Sodoma na Gomora, na zambi yao ni kubwa sana.


Yawe Mungu akamwuliza yule mwanamuke: “Umefanya nini wewe?” Mwanamuke akamujibu: “Nyoka alinidanganya, nami nikakula.”


Damu ya uzima wenu nitaidai. Nitaidai kutoka kwa kila nyama na mwanadamu. Atakayemwua mwanadamu mwenzake, nitamudai uzima wake.


Yawe alisema: ‘Kwa ile damu ya Naboti na kwa damu ya wana wake niliyoona jana, nitakulipiza kisasi katika shamba hilo.’ Ni ujumbe wa Yawe. Kwa hiyo, kamata maiti ya Yoramu uitupe katika shamba la Naboti kama vile Yawe alivyosema.”


Lakini kule Samaria kulikuwa nabii wa Yawe, jina lake Obedi. Yeye alitoka kwenda kukutana na waaskari wa Israeli walipokuwa karibu kuingia Samaria, akawaambia: “Yawe, Mungu wa babu zenu, alikuwa amewakasirikia watu wa Yuda, ndiyo maana aliwatia katika mikono yako lakini umewaua kwa hasira. Tendo hilo limetoka mbinguni.


Ewe dunia, usifunike damu yangu iliyomwangika; kilio changu kienee kila pahali.


Kutoka katika muji, kilio cha wanaokufa kinasikilika, na walioumizwa wanalalamika kuomba musaada. Lakini Mungu hasikilizi kabisa maombi yao.


Umefanya hayo yote nami nimenyamaza. Unazani kwamba mimi ni kama wewe? Lakini sasa nitakukaripia, nitakugombeza waziwazi.


Atawatoa katika mateso na ukali, maana maisha yao ni ya bei kubwa kwake.


Mumwimbie sifa Yawe anayekaa Sayuni! Muyatangazie mataifa mambo aliyotenda!


Mungu analipiza kisasi cha damu iliyomwangwa; wala hasahau hata kidogo kilio cha wenye kuonewa.


Kisha Yawe akamwambia: “Nimeona mateso ya watu wangu wanaokuwa katika inchi ya Misri na nimesikia kilio chao kinachosababishwa na watesaji wao. Ninajua mateso yao,


Shamba la mizabibu la Yawe wa majeshi ni taifa la Waisraeli, na mizabibu mizuri aliyoipanda ni watu wa Yuda. Yeye alitazamia watu wafuate sheria yake, akaona mauaji; alitazamia haki, alisikia kilio!


Mukifanya hivyo mutachafua inchi ambayo munakaa ndani yake. Umwangaji wa damu unachafua inchi, na hakuna sadaka inayoweza kutakasa inchi iliyofanyiwa mauaji isipokuwa kwa kumwua mwuaji huyo.


Basi Petro akamwuliza: “Anania, namna gani Shetani amekuingia hata akakusemesha uongo mbele ya Roho Mutakatifu na kuficha sehemu ya feza ulizopata ulipouzisha lile shamba?


Halafu Petro akamwambia: “Namna gani mulipatana kwa kumupima Roho wa Bwana? Sikiliza! Wale wanaotoka kumuzika mume wako wamefika hapa kwenye mulango, nao watakupeleka vilevile.”


“Mutu akipatikana ameuawa katika mbuga katika inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapa kuwa urizi wenu, nanyi hamujui ni nani aliyemwua,


Kwa njia ya imani, Abeli alimutolea Mungu sadaka nzuri zaidi kuliko ile ya Kaina. Kwa ajili ya imani yake alihesabiwa na Mungu kuwa mwenye haki, kwa maana Mungu mwenyewe alikubali sadaka zake. Na kwa imani ile, ingawa Abeli amekwisha kufa, angali anasema.


Mumefikia karibu na Yesu anayekuwa mupatanishi wa agano jipya, na kwenye damu yake iliyomwangwa inayosema nasi maneno mema zaidi kuliko damu ya Abeli.


Ninyi hamukulipa mishahara ya watumishi waliotumika katika mashamba yenu. Musikilize mashitaki yao! Malalamiko ya wavunaji yamefika katika masikio ya Bwana Mwenye Uwezo!


Yoshua akamwambia Akana: “Mwana wangu, umutukuze Yawe, Mungu wa Israeli, umusifu na kisha uniambie yale uliyotenda, wala usinifiche.”


Samweli akamwuliza: “Umefanya nini?” Saulo akamujibu: “Nilipoona watu wananiacha, na wewe haukukuja katika muda wa siku ulizosema, na tena nilipoona Wafilistini wamejipanga tayari kwa vita kule Mikimasi,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ