Mwanzo 39:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
4 Basi, Yosefu akapata kukubaliwa mbele ya Potifari, hata akakuwa mutumishi wake wa pekee. Akamufanya musimamizi wa nyumba yake na mwangalizi wa mali yake yote.
Ni kweli kwamba mimi mutumishi wako nimepata kukubaliwa mbele yako, nawe umenitendea mema sana kwa kuokoa maisha yangu. Lakini kwenye milima ni mbali sana. Maangamizi haya yatanikuta mbele sijafika kule, nami nitakufa.
Yakobo akamwambia: “Hapana! Kama kweli nimekubaliwa mbele yako, ninakusihi uipokee zawadi yangu. Hakika, kuona uso wako ni kama kuona uso wa Mungu, kwa vile ulivyonipokea kwa wema mukubwa.
Halafu Esau akauliza: “Kundi lile nililokutana nalo katika njia lina maana gani?” Yakobo akamujibu: “Nilitumaini kupata kukubaliwa mbele yako, ee bwana wangu.”
Lakini Yosefu akakataa na kumwambia yule muke wa bwana wake: “Sikiliza! Bwana wangu amenipa mamlaka juu ya kila kitu hapa ndani ya nyumba na hajishugulishi na kitu chochote tena.
Jemadari wake Simuri ambaye alisimamia nusu ya kundi ya magari yake ya vita alimwasi. Siku moja, mufalme Ela alipokuwa kule Tirza katika nyumba ya Arsa aliyekuwa musimamizi wa nyumba ya kifalme, alikunywa, akalewa.
Hegayi akapendezwa na Esteri hata kiasi cha kumupendelea. Bila kupoteza wakati, akamupa Esteri mafuta na chakula. Vilevile, akamuhamishia pahali pazuri kabisa katika nyumba hiyo ya wanawake, akamuchagulia wajakazi saba kutoka nyumba ya mufalme.
Mujichunge ninyi wenyewe na muchunge vilevile lile kundi lote Roho Mutakatifu alilowapatia kusudi mukuwe wasimamizi wao. Hivi mutaweza kuchunga kanisa la Mungu ambalo alijipatia kwa damu ya Mwana wake.