Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 39:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Yule bwana wake akatambua kwamba Yawe alikuwa pamoja na Yosefu, na kwamba ndiye aliyefanikisha mambo yote Yosefu aliyofanya.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 39:3
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu akakuwa pamoja na yule mutoto, naye akaendelea kukomaa. Alikaa katika jangwa na akakuwa mupiga upinde hodari sana.


Wakati ule, Abimeleki pamoja na Fikoli, jemadari wa jeshi lake, akamwendea Abrahamu, akamwambia: “Mungu yuko pamoja nawe katika kila kitu unachofanya.


Kwa hiyo uniapie kwa jina la Mungu kwamba hautanidanganya mimi au watoto wangu au wazao wangu. Kadiri mimi nilivyokutendea mema, vivyo hivyo nawe unitendee mema mimi na inchi hii unamokaa.”


Usiku uleule Yawe alimutokea na kumwambia: “Mimi ni Mungu wa baba yako Abrahamu. Usiogope; niko pamoja nawe. Nitakubariki na kuwazidisha wazao wako kwa ajili ya Abrahamu, mutumishi wangu.”


Wao wakamujibu: “Tumeona wazi kwamba Yawe yuko pamoja nawe. Kwa hiyo, tunafikiri inafaa tufanye kiapo pamoja nawe na kufanya agano,


Lakini Labani akamwambia: “Basi uniruhusu nami niseme. Nimetambua kwa kuaguza kwamba Yawe amenibariki kwa sababu yako.


Mbele sijakuja ulikuwa na mali chache tu lakini tangu nifike, mali yako imeongezeka kwa wingi sana, na Yawe amekubariki kila fasi nilikokwenda. Lakini sasa, nitatunza wakati gani jamaa yangu mwenyewe?”


Yawe alikuwa pamoja na Yosefu, akamufanikisha sana. Yosefu akakuwa anakaa katika nyumba ya bwana wake Mumisri.


Yawe alikuwa pamoja na Yosefu na kumutendea mema, hata kumufanya apate kukubaliwa mbele ya mukubwa wa kifungo.


Yule mukubwa wa kifungo hakujishugulisha tena na kitu chochote Yosefu alichopewa kwa maana Yawe alikuwa pamoja na Yosefu na kufanikisha kila kitu alichofanya.


Basi, Yawe alikuwa pamoja naye, na alimwezesha kwa kila jambo alilotenda. Alimwasi mufalme wa Asuria na kukataa kumutumikia.


Ukiwa mwangalifu, na ukitii masharti na maagizo ambayo Yawe alimwagiza Musa juu ya Israeli, utastawi. Ujipe moyo, ukuwe imara. Usiogope wala usifazaike.


Finehasi mwana wa Eleazari, alikuwa musimamizi wao, zamani, Yawe alikuwa pamoja naye.


Solomono, mwana wa mufalme Daudi, alijiimarisha katika utawala wake, naye Yawe, Mungu wake akamubariki na kumufanya akuwe mukubwa sana.


Akamutumikia Yawe kwa uaminifu wakati wa kuishi kwa Zakaria, aliyemufundisha kumutii Mungu. Kwa jinsi alivyomutafuta Mungu, Mungu alimufanikisha.


Nikawajibu: “Mungu wa mbinguni atatufanikisha katika kazi hii, nasi tunaokuwa watumishi wake tutaanza kujenga. Lakini ninyi hamuna sehemu au haki wala ukumbusho katika Yerusalema.”


Huyo ni kama muti uliopandwa kando ya vijito, unaozaa matunda kwa wakati wake, na majani yake hayanyauki hata kidogo. Anafanikiwa katika yote anayofanya.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Wakati ule, watu kumi kutoka mataifa ya kila luga watamukamatilia Muyuda mumoja na kushika nguo yake na kumwambia: Tunataka kwenda pamoja nanyi, kwa sababu tumesikia kwamba Mungu yuko pamoja nanyi.


Vilevile, mwangaza wenu unapaswa kuangaza mbele ya watu, kusudi waone matendo yenu mazuri, nao wamutukuze Baba yenu anayekuwa mbinguni.


Kila siku ya kwanza ya juma, kila mumoja wenu anapaswa kuweka akiba ya mali kwake, kwa kadiri ya mapato yake, kusudi musihitaji kufanya muchango wakati nitakapokuja.


“Basi, mukumbuke jinsi Yawe Mungu wenu alivyowabariki ninyi katika kila jambo mulilofanya. Aliwatunza mulipokuwa munatangatanga katika jangwa hili kubwa. Amekuwa pamoja nanyi miaka hii yote makumi ine na hamukupungukiwa na kitu chochote.


Kumbuka kwamba mimi nimekuamuru ukuwe imara na hodari. Usiogope wala usifazaike kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, niko pamoja nawe popote utakapoenda.”


Angalia, nitakupa watu wa kikundi chenye kuabudu Shetani, ndio wale wasema uongo wanaojidai kwamba wao ni Wayuda, lakini ni wadanganyifu. Hakika nitawalazimisha kupiga magoti mbele yako, nao watajua ya kuwa mimi ninakupenda.


Daudi alifanikiwa katika kila kitu alichofanya, maana Yawe alikuwa pamoja naye.


Lakini Saulo alipoona wazi kwamba Yawe alikuwa pamoja na Daudi, na kwamba Mikali binti yake alimupenda sana Daudi,


Samweli aliendelea kukomaa na Yawe akakuwa pamoja naye, na yale yote aliyosema hakuna hata moja ambalo halikutimia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ