Mwanzo 39:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
14 akaita watumishi wa nyumba yake na kuwaambia: “Huyu Mwebrania tuliyeletewa anatuzarau. Alikuja kwangu akitaka kunishika kwa nguvu, lakini nikapiga kelele.
Mutu mumoja aliyeponyoka, akakwenda kumwarifu Abramu Mwebrania ambaye alikuwa anaishi karibu na mielo ya Mamure Mwamori. Mamure alikuwa ndugu ya Eskoli na Aneri. Wote walikuwa wamefanya agano na Abramu.
Silaha zote zilizotengenezwa kwa kukuzuru wewe hazitafaa kwa kitu chochote. Mutu akikushitaki, utamushinda. Hiyo ndiyo haki niliyowapangia watumishi wangu. Hizo ndizo haki nilizowahakikishia. –Ni ujumbe wa Yawe.
Wakaanza kumushitaki, wakisema: “Tulimukuta mutu huyu akiwashawishi watu wa taifa letu kufanya uasi. Yeye alikuwa akiwaambia kwamba wasilipe kodi kwa Mufalme wa Roma. Na zaidi ya hii anasema kwamba yeye ndiye Kristo, Mufalme aliyengojewa.”
Kuna sifa gani kama mukivumilia mapigo kwa sababu mulitenda mabaya? Lakini mukivumilia mateso kwa sababu mulitenda mema, jambo hilo linamupendeza Mungu.