Mwanzo 38:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
9 Lakini Onani alijua kwamba hao watoto hawangekuwa wake. Kwa hiyo, alipolala na muke wa ndugu yake, alimwanga chini mbegu ya uzazi, kusudi asimupatie ndugu yake watoto.
“Kama wandugu wanaishi pahali fulani na mumoja wao akikufa bila kuacha mutoto mwanaume, muke wa marehemu asiolewe na mutu mwingine inje ya jamaa hiyo. Yule ndugu wa marehemu anapaswa kumwoa mujane huyo.
Kwa maana zamani sisi vilevile tulikuwa wajinga, waasi na wapotovu. Tulikuwa tumetawaliwa na kila namna ya tamaa mbaya na ya vitu mbalimbali vilivyotuvuta sana. Tuliishi katika uovu na wivu, tuliwachukiza watu nao walituchukia.
Zaidi ya hayo, nimemupata Ruta wa Moabu mujane wa Malona, kusudi akuwe muke wangu. Mapatano haya yatafanya mali ya jamaa ya marehemu na ukoo wake kubakia kwa watu wake katika muji huu. Ninyi ni washuhuda.”