Yuda na wana wake: Eri, Onani, Sela, Peresi na Zera. (Lakini Eri na Onani walikufa katika inchi ya Kanana). Wana wa Peresi walikuwa Hesironi na Hamuli.
Wana wa Yuda walikuwa watano: Wana wa Yuda aliozaliwa na Beti-Sua, muke wake Mukanana, walikuwa: Eri, Onanu na Sela. Eri, muzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu mbele ya Yawe, basi Yawe akamwua. Na Tamari, muke wake alimuzalia wana wawili: Peresi na Zera.
Na aliwatoa wana wake kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto katika bonde la mwana wa Hinomu. Alipiga ramuli, aliaguza na alitumia hirizi; hata alishirikiana na waaguzi wanaosemezana na mizimu na wachawi. Alitenda maovu mengi mbele ya Yawe, akamukasirikisha.
Mutu akimukosea mwenzake, anaweza kuombewa kwa Mungu, kusudi Mungu amusamehe. Lakini mutu akimukosea Yawe nani anayeweza kumwombea musamaha?” Lakini watoto hao hawakumusikiliza baba yao, maana Yawe alikwisha kata shauri la kuwaua.