Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 38:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Kisha miezi mitatu, Yuda akapata habari hii: “Tamari, muke wa mwana wako amekuwa kahaba, tena amepata mimba kwa kufanya ukahaba.” Basi, Yuda akaamuru: “Mumutoshe inje achomwe kwa moto!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 38:24
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Mungu akamufikia Abimeleki katika ndoto usiku, akamwambia: “Wewe utakufa kwa sababu ya mwanamuke uliyemutwaa, maana yuko na mume wake.”


Sasa umurudishe yule mwanamuke kwa mume wake. Abrahamu ni nabii. Atakuombea nawe utaishi. Lakini usipomurudisha, ujue kwa hakika kwamba wewe utakufa pamoja na watu wako wote.”


Kwa hiyo Abimeleki akamwita Abrahamu, akamwuliza: “Umetutendea nini? Nimekukosea nini hata ukaniletea zambi kubwa, mimi na ufalme wangu? Umenitendea mambo yasiyostahili kutendwa.”


Hao wandugu wawili wakajibu: “Ana haki gani ya kumutendea dada yetu kama kahaba?”


Yuda akasema: “Acha avichukue vitu hivyo. Kama sivyo atatufanya tuchekelewe. Wewe mwenyewe umeona kwamba nilimupelekea mwana-mbuzi, lakini wewe haukumupata.”


Daudi aliposikia hayo, akawaka hasira juu ya yule tajiri. Akamwambia nabii Natani: “Kama vile Yawe anavyoishi, mutu aliyefanya jambo hilo anastahili kufa!


Natani akamwambia Daudi: “Wewe ndiwe mutu yule! Sasa, Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Mimi nilikupakaa mafuta ukuwe mufalme juu ya Israeli. Nilikuokoa toka katika mikono ya Saulo.


Jambo moja nililotambua linalokuwa baya zaidi kuliko kifo, ni mwanamuke ambaye moyo wake ni mutego na wavu, na mikono yake ni kama minyororo. Lakini anayemupendeza Mungu anamwepuka mwanamuke yule, lakini mwenye zambi ananaswa naye.


Yawe anasema: Tangu zamani wewe ulivunja nira yako, ulikata minyororo yako, ukasema: “Sitakutumikia”. Juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila muti wa majani mabichi, ukalala machali kama kahaba.


Mume akiachana na muke wake, naye muke akijiendea, na kuolewa na mwingine, mume yule anaweza kumurudilia muke huyo? Kufanya hivyo hakutaichafua inchi kabisa? Wewe Israeli, umefanya ukahaba na wapenzi wengi, sasa unataka kunirudilia mimi? –Ni ujumbe wa Yawe.–


Katika siku ya utawala wa mufalme Yosia, Yawe aliniambia hivi: Umeona jinsi yule Israeli asiyekuwa mwaminifu alivyofanya? Aliniacha, akapanda juu ya kila kilima kirefu na kwenda chini ya kila muti wenye majani mabichi, akafanya ukahaba wake kule!


Zaidi ya hayo, Yuda alishuhudia kwamba niliachana na Israeli kwa sababu ya ukahaba wake na kwa kukosa uaminifu kwangu. Lakini hata hivyo, Yuda, dada yake mudanganyifu, hakuogopa; naye vilevile alikwenda na kufanya ukahaba!


Lakini, ulitegemea uzuri wako, ukatumia sifa yako kwa kufanya uzinzi, ukifanya ukahaba na mutu yeyote anayepita.


Kwa mwanzo wa kila barabara ulijijengea nafasi inayoinuka, ukautumia uzuri wako kwa kufanya uzinzi ukijitoa kwa kila mupita njia na kuongeza uzinzi wako.


Tena ulifanya uzinzi na jirani zako Wamisri waliojaa tamaa, ukaongeza uzinzi wako na kuichochea hasira yangu.


Kwa sababu haukutosheka, ulifanya tena uzinzi na Waasuria. Na hiyo vilevile haikukutoshelea.


Nyumba zako wataziteketeza kwa moto na kuwafanya wanawake wengi waone azabu yako. Utakoma kujitoa kwa mutu yeyote afanye uzinzi nawe.


Hata hivyo, akazidisha uzinzi wake akifanya kama wakati wa ujana wake alipofanya uzinzi kule Misri.


Kila mumoja alimwendea kama wanaume wanavyomwendea kahaba. Ndivyo walivyowaendea Ohola na Oholiba wale wanawake waasherati.


Ingawa Ohola alikuwa muke wangu, lakini aliendelea kuwa muzinzi na kuwatamani wapenzi wake Waasuria.


Kama sivyo, nitamuvua nguo abaki uchi, nitamufanya akuwe sawa vile alivyozaliwa. Nitamufanya akuwe utupu sawa jangwa, akauke sawa inchi kavu. Nitamwua kwa kiu.


Kisha nikamwambia: Unapaswa kuwa wangu kwa siku nyingi bila kufanya uzinzi au kuwa muke wa mutu mwingine; nami vilevile nitakuwa mwaminifu.


Ikiwa kweli ninyi Waisraeli ni wazinzi lakini, watu wa Yuda basi wasianguke ndani ya makosa! Musiende pahali patakatifu kule Gilgali, wala musiende kule Nyumba ya Uovu. Wala musiape mukisema: Kama vile Yawe anavyoishi!


Kama mwanaume akifanya uzinzi na muke wa mwenzake, wote wawili wanapaswa kuuawa.


Binti wa kuhani yeyote akijichafua kwa kufanya ukahaba, atateketezwa kwa moto maana anamuchafua baba yake.


Ulinde kwa ajili yako mwenyewe kile unachoaminia juu ya mambo yale mbele ya Mungu. Heri mutu asiyejihukumu katika kusudi lake.


“Wazazi wasiuawe kwa makosa ya watoto wao, wala watoto wasiuawe kwa ajili ya makosa ya wazazi wao. Kila mutu atauawa kwa makosa yake mwenyewe.


Lakini habara yule akamukasirikia yule Mulawi, akamwacha na kurudi katika nyumba ya baba yake kule Betelehemu, akakaa kwa muda wa miezi mine.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ