akavua nguo zake za ujane na kujifunika kitambaa. Kisha akaikaa kwenye mulango wa kuingilia Enaimu, kijiji kilichokuwa katika njia kwenda Timuna. Alifanya hivyo kwa vile aliona kwamba Sela alikwisha kuwa mutu muzima, lakini yeye Tamari hakuoeshwa akuwe muke wake.
Yuda akamwuliza: “Unataka nikupe nini kama rehani?” Naye akamujibu: “Unipe hiyo pete na kamba yake pamoja na hiyo fimbo unayoshika.” Basi, Yuda akamupa vitu hivyo vyote, akalala naye. Tamari akapata mimba yake.
Kwa hiyo alituma watu kule Tekoa kusudi wamutafutie mwanamuke mwenye hekima. Walipomuleta, akamwambia: “Ujifanye sawa vile mwenye kuwa na kilio. Vaa nguo za kilio, usijipakae mafuta, lakini ujifanye kama mwanamuke ambaye amekuwa katika kilio kwa muda murefu.