Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 38:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Yuda akamujibu: “Nitakupa mwana-mbuzi kutoka kundi langu.” Tamari akamwambia: “Weka rehani kwa kuhakikisha kwamba utaniletea yule mwana-mbuzi.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 38:17
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu, bila kujua kwamba huyo alikuwa muke wa mwana wake, akamwendea pale kando ya njia, akamwambia: “Ninataka kulala nawe.” Tamari akamwuliza: “Utanipa nini upate kulala nami?”


Yuda akamwuliza: “Unataka nikupe nini kama rehani?” Naye akamujibu: “Unipe hiyo pete na kamba yake pamoja na hiyo fimbo unayoshika.” Basi, Yuda akamupa vitu hivyo vyote, akalala naye. Tamari akapata mimba yake.


Wakati Yuda alipomutuma yule rafiki yake, Mwadulami, amupelekee yule mwanamuke mwana-mbuzi kusudi arudishiwe rehani aliyomwachia, Hira hakumupata.


Mutu akiahidi kumukopesha mutu asiyejulikana, unyanganye nguo yake kuwa rehani.


Kwa kawaida wanaume wanawalipa makahaba, lakini wewe umewalipa wapenzi wako wote, ukiwahonga wakuje kwako toka pande zote upate kuzini nao.


Basi bwana wa yule mulinzi akamusifu kwa sababu alitenda kwa werevu. Kwa maana watu wa dunia hii wanatengeneza maneno yao na wenzao kwa werevu sana kuliko watu wanaopenda kuishi katika mwangaza.”


Nyuma ya muda fulani, wakati wa mavuno ya ngano, Samusoni akatwaa mwana-mbuzi, akaenda kumutembelea muke wake. Akamwambia baba mukwe wake kwamba anataka kumwona muke wake ndani ya chumba chake. Lakini baba mukwe hakumuruhusu,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ