19 Wakaambiana: “Muangalie! Yule mwota ndoto anakuja.
Akaota ndoto, na katika ndoto hiyo, aliona ngazi iliyosimamishwa juu ya dunia na incha yake inafika mbinguni. Wamalaika wa Mungu walikuwa wakipanda na kushuka katika ngazi hiyo.
Wandugu zake wakamwonea wivu, lakini baba yake akakuwa anafikiri juu ya jambo hilo.
Wandugu zake walipomwona akiwa mbali na mbele hajafika karibu, wakafanya mupango wa kumwua.
Basi, tumwue na kumutupa ndani ya shimo moja. Kisha tutasema kwamba ameuawa na nyama wa pori. Halafu tutaona hizo ndoto zake zitakuwa namna gani.”
Usiku mumoja, Yosefu akaota ndoto, lakini alipowaelezea wandugu zake, wao wakazidi kumuchukia.
Wapiga mishale walimushambulia vikali, wakamutupia mishale na kumusumbua sana.