Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 37:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Wandugu zake walipomwona akiwa mbali na mbele hajafika karibu, wakafanya mupango wa kumwua.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 37:18
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Esau akamuchukia Yakobo kwa sababu ya baraka aliyokuwa amepewa na baba yake. Esau akawaza: “Siku za kilio cha baba zitakapokwisha, ndipo nitakapomwua ndugu yangu Yakobo.”


Wakaambiana: “Muangalie! Yule mwota ndoto anakuja.


Nyuma ya kifo cha baba yao, wandugu za Yosefu walisemezana: “Labda Yosefu atatuchukia na kutulipiza mabaya yote tuliyomutendea.”


Ninyi mulitaka kunitendea vibaya, lakini Mungu alikusudia mema kusudi watu wengi wapate kuwa wazima kama vile munavyoona leo.


Aliwafanya Wamisri wawachukie watu wake, wakawatendea watumishi wake vibaya.


Ingawa niliwapenda, walinishitaki. Hata hivyo, niliwaombea.


Nimesahaulika kama mutu aliyekufa; nimekuwa kama chungu kilichovunjikavunjika.


Ninasikia watu wakinongonezana; kuna vitisho kila upande. Wanafanya shauri baya juu yangu, wanafanya mipango ya kuniua.


Mwovu anamufanyia mutu wa haki shauri baya, na kumusagia meno kwa chuki.


Mutu mwovu anamuvizia mutu wa haki, na kujaribu kumwua;


Wao wanapatana kuwaangamiza watu wa haki, na kuwahukumu watu wasiokuwa na kosa wauawe.


Lakini wakati walimaji walipomwona yule mwana, wakasemezana: ‘Musimame! Huyu ndiye atakayerizi shamba hili. Basi tumwue, na shamba hili litakuwa urizi wetu!’


Kulipokucha, wakubwa wote wa makuhani na wasimamizi wa watu wakakata shauri la kumwua Yesu.


Lakini wale walimaji walipomwona akikuja, wakasemezana: ‘Musimame! Huyu ndiye atakayerizi shamba hili. Basi tumwue, na shamba hili litakuwa urizi wetu!’


Kulikuwa kumebaki siku mbili mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka na ya Mukate Usiyotiwa Chachu. Wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria walitafuta njia ya kumukamata Yesu kwa werevu kusudi wamwue.


Basi tangia siku ile wakakusudia kumwua Yesu.


Kesho yake kulipokucha, Wayuda wakafanya shauri; wakafanya kiapo kwamba hawatakula wala kunywa mpaka wamwue Paulo kwanza.


Saulo alimwelezea mwana wake Yonatani na wakubwa wake juu ya mupango wake wa kumwua Daudi. Lakini Yonatani, mwana wa Saulo, alimupenda sana Daudi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ