Labani akamwambia: “Karibu kwetu wewe uliyebarikiwa na Yawe. Mbona unasimama inje? Mimi mwenyewe nimekwisha tayarisha nyumba na pahali kwa ajili ya hawa ngamia wako!”
Ee Yawe umeinua mukono kwa kuwaazibu, lakini hawauoni. Uwaonyeshe namna unavyowapenda watu wako nao watapata haya. Moto unaowatayarishia waadui zako, uwateketeze!
Huu ndio mwisho wa jambo hilo. Mawazo yangu yaliniogopesha sana mimi Danieli, hata rangi yangu ikabadilika. Lakini nilichunga jambo hilo ndani ya moyo wangu.
chuki, uuaji, ulevi, ulafi, na mambo mengine yanayofanana na hayo. Ninawaonya tena kama vile nilivyowaonya mbele, kwamba watu wanaotenda mambo kama hayo hawatashiriki katika Ufalme wa Mungu.
Kwa maana zamani sisi vilevile tulikuwa wajinga, waasi na wapotovu. Tulikuwa tumetawaliwa na kila namna ya tamaa mbaya na ya vitu mbalimbali vilivyotuvuta sana. Tuliishi katika uovu na wivu, tuliwachukiza watu nao walituchukia.
Saulo hakupendezwa na maneno ya wimbo huo. Akakasirika sana. Akasema: “Wamemupa Daudi elfu makumi, lakini mimi wamenipa maelfu tu. Linalobakia ni kumupa Daudi ufalme.”