Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 37:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Lakini alipomwelezea baba yake na wandugu zake ndoto hiyo, baba yake alimukaripia, akisema: “Ni ndoto gani hiyo uliyoota? Itatupasa mimi, mama yako na wandugu zako kuja kuinama chini kwa heshima mbele yako?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 37:10
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Jamii za watu zikutumikie, na mataifa yainame mbele yako kwa heshima. Ukuwe mutawala wa wandugu zako, na wana wa mama yako wainame mbele yako kwa heshima. Kila mutu anayekulaani alaaniwe, kila mutu anayekubariki abarikiwe!”


Niliota kwamba sisi wote tulikuwa katika shamba tukifunga miganda. Kwa rafla muganda wangu ukainuka na kusimama wima. Miganda yenu ikakusanyika kuuzunguka na kuinamia mbele ya muganda wangu.”


Kisha Yosefu akaota ndoto ingine, akawaelezea wandugu zake akisema: “Musikilize, nimeota ndoto nyingine. Nimeona jua, mwezi na nyota kumi na moja vinainamia mbele yangu.”


Yosefu, aliporudi kwake, wakamuletea zile zawadi walizokuwa nazo, wakainama mbele yake kwa heshima.


Wakamujibu: “Mutumishi wako, baba yetu, yuko salama na angali muzima.” Kisha wakainama kwa heshima.


Yuda na wandugu zake wakafika kwa Yosefu naye Yosefu alikuwa bado katika nyumba. Basi, wakainama mbele yake kwa heshima,


Wazao wa wale waliokutesa, watakuja na kuinama uso mpaka chini mbele yako. Wote wale waliokuzarau, watapiga magoti kwenye miguu yako. Watakuita: “Muji wa Yawe”, “Sayuni”, “Muji wa Mutakatifu wa Israeli”.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ