Kwa hiyo Esau akamwambia Yakobo: “Ninasikia njaa. Tafazali, unigawanyie muchuzi huo mwekundu nikule.” Ndiyo maana walimupanga jina Edomu, maana yake “mwekundu”.
Magdieli na Iramu. Hao ndio wakubwa wa makabila yaliyotokana na Edomu, maana yake, Esau, baba ya Edomu. Wametajwa kulingana na makao yao katika sehemu za inchi walizorizi.
Sasa Waamoni, Wamoabu na watu wa mulima Seiri, ambao haukuwaruhusu babu zetu washambulie inchi zao walipotoka Misri, wakapitia kandokando wasiwaangamize,
Waamoni na Wamoabu wakawashambulia wenyeji wa mulima Seiri, na kuwaangamiza kabisa. Kisha kuwaangamiza wakaaji wa mulima Seiri wakaanza kushambuliana wao kwa wao, wakaangamizana.
Vilevile Wayuda waliokuwa katika inchi ya Moabu na kati ya Waamoni na katika inchi ya Edomu na inchi zingine, waliposikia kwamba mufalme wa Babeli amewaruhusu Wayuda wengine kubaki katika inchi ya Yuda na kwamba amemusimika Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu kuwa mutawala wao,
Haya ni maono ya Obadia. Bwana wetu Yawe anasema hivi juu ya taifa la Edomu. Tumepata habari kutoka kwa Yawe; mujumbe ametumwa kati ya mataifa: Musimame! Tuende tupigane na taifa la Edomu!
Kiburi chako kimekudanganya: wewe unayekaa ndani ya mashimo chini ya mawe makubwa na makao yako yapo juu kwenye milima, hivyo unajisemesha: Nani anayeweza kunishusha chini?
Yawe akafanya kama vile alivyowafanyia wazao wa Esau ndio Waedomu, ambao wanaishi katika inchi ya Seiri. Aliwaangamiza Wahori wakati Waedomu walipofika huko, wakanyanganya inchi yao na kuishi humo mpaka leo.
musipigane nao kwa sababu sitawapa sehemu yoyote ya inchi yao. Sitawapa hata pahali padogo pa kukanyaga. Inchi hiyo ya milima ya Seiri nimewapa wazao wa Esau ikuwe mali yao.
Saulo alipokwisha kuwa mufalme wa Waisraeli, alipigana na waadui zake wote kila upande: Wamoabu, Waamoni, Waedomu, wafalme wa Zoba na Wafilistini. Kila mara alipopigana vita, alishinda.