Wana wa Oholibama, muke wa Esau, walikuwa Yeusi, Yalamu na Kora. Kila mumoja wao akiwa mukubwa wa kabila lake. Hao wote ni wana wa Oholibama, binti ya Ana, muke wa Esau.
Kisha, Esau akawatwaa wake zake, watoto wake wanaume na wanawake, watu wote wa nyumba yake, ngombe wake, nyama wake wengine wote na mali yake yote ambayo alikuwa ameipata katika inchi ya Kanana, akahamia pahali pengine, mbali na ndugu yake Yakobo.