Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 34:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 na wakati uleule wana wa Yakobo walirudi kwa nyumba kutoka kwenye malisho. Waliposikia hayo, vijana wale wakaona uchungu mwingi na kukasirika sana, kwa vile Sekemu alikuwa amewafanyia watu wa Israeli ovu hilo la kulala na binti ya Yakobo; maana jambo hilo halipaswi kutendwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 34:7
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo Abimeleki akamwita Abrahamu, akamwuliza: “Umetutendea nini? Nimekukosea nini hata ukaniletea zambi kubwa, mimi na ufalme wangu? Umenitendea mambo yasiyostahili kutendwa.”


Hamori, baba ya Sekemu, akakwenda kwa Yakobo kusudi azungumuze naye,


Lakini Hamori akawaambia: “Mwana wangu Sekemu anamupenda sana binti yenu. Basi, tafazali mumuruhusu amwoe.


wana wake, wajukuu wake wanaume na wanawake. Wote akawaleta Misri.


Mufalme Daudi aliposikia jambo hilo alikasirika sana.


Ee Yawe, maagizo yako ni imara; nyumba yako ni takatifu milele.


nikawaona vijana wengi wajinga, na hasa mumoja aliyekuwa mupumbafu.


Jambo hili litawafikia kwa sababu wametenda katika Israeli mambo yasiyofanyika. Walizini na wake za jirani zao, na kusema maneno ya uongo kwa jina langu, jambo ambalo mimi sikuwaamuru wafanye. Mimi ninajua hayo. Nimeyashuhudia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Ikiwa Waisraeli wote pamoja wametenda zambi bila kukusudia kwa kufanya kitu kilichokatazwa na amri ya Yawe,


Uwaambie watu wa Israeli hivi: Kama mutu akitenda zambi bila kukusudia, akifanya kitu kilichokatazwa na amri ya Yawe, atafanya hivi:


Kama mutu wa kawaida ametenda zambi bila kukusudia, kwa kufanya kitu kilichokatazwa na amri ya Yawe na hivyo akakuwa na kosa,


Musifanye uasherati kama vile wamoja kati yao walivyofanya hata wakakufa kwa siku moja watu elfu makumi mbili na tatu.


Muepuke uzinzi! Zambi ingine yoyote mutu anayofanya haigusi mwili wake, lakini yule anayefanya uzinzi anafanya zambi juu ya mwili wake mwenyewe.


Kama vile inavyowapasa watu wa Mungu kuishi, tendo lolote la uasherati, la uchafu wala la tamaa ya mali lisisikilike kati yenu.


Lakini kama mashitaki hayo ni ya kweli, na hakuna ushuhuda wa ubikira wake,


watamupeleka kwenye mulango wa nyumba ya baba yake na wanaume wa muji huo watamupiga mawe akufe, kwa sababu amefanya upumbafu katika Israeli kwa kufanya ukahaba akiwa katika nyumba ya baba yake. Ndivyo mutakavyokomesha uovu huo kati yenu.


Ataishi pamoja nawe pahali atakapochagua katika moja ya makao yako, pahali panapomupendeza. Usimutese.


Basi mutupilie mbali mambo yote ya kidunia yanayokuwa ndani yenu: uasherati, uchafu, nia mbaya, tamaa mbaya na tamaa ya mali inayokuwa sawa vile kuabudu sanamu.


Na zaidi ya hiyo, wanashikwa na uvivu na kuwa na tabia ya kutangatanga nyumba kwa nyumba. Na si ile tu, vilevile wao ni wakatetea na wenye kujiingiza katika maneno ya watu wengine na kusema maneno yasiyofaa.


Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, mume na muke wake wanapaswa kujikinga na uchafu, kwa sababu Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati.


Ndani ya kinywa kimoja munatoka maneno ya sifa na ya laana. Wandugu zangu, mambo haya hayapaswi kuwa vile.


Mutu yeyote atakayepatikana akiwa na vitu vilivyotolewa viangamizwe atateketezwa kwa moto, yeye pamoja na kila kitu chake maana ameliasi agano langu mimi Yawe, akatenda jambo la haya katika Israeli.’ ”


Lakini ninyi ni watu wa kizazi kilichochaguliwa na Mungu na wa ukuhani wa kifalme. Ninyi ni taifa takatifu na watu wa pekee wa Mungu. Mumechaguliwa kusudi mutangaze matendo makubwa ya yule aliyewaita kutoka katika giza na kuwaingiza kwenye mwangaza wake wa ajabu.


Mimi nikabeba maiti yake, nikamukatakata vipande na kuvipeleka kwa makabila yote ya Israeli, maana wamefanya jambo la kuchukiza na potovu katika Israeli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ