Wewe unawapenda wale wanaokuchukia na unawachukia wale wanaokupenda. Umetuonyesha waziwazi leo kwamba majemadari na watumishi wako hawana maana kwako. Ninaona leo, kama Abusaloma angekuwa muzima, na sisi wote tungalikufa, ungeona ni sawa.
Mufalme Hezekia aliwasifu na kuwatia moyo makuhani kwa sababu waliendesha ibada kwa ujuzi mwingi. Nyuma ya kumaliza siku saba ambamo watu walikula, wakatoa sadaka za amani na kumutukuza Yawe, Mungu wa babu zao,
Museme na watu wa Yerusalema kwa upole, muwaambie kwamba utumwa wao umekwisha, wamesamehewa uovu wao. Yawe amewaazibu mara mbili kwa sababu ya zambi zao zote.
Siku moja, mume wake akakwenda kumutafuta. Alikusudia kuongea naye vizuri na kumurudisha kwa nyumba yake. Akakwenda pamoja na mutumishi wake na punda wawili. Basi yule mwanamuke akamupeleka ndani kwa baba yake, naye baba mukwe alipomwona akamupokea kwa furaha.
Saulo alipomaliza kuzungumuza na Daudi, Yonatani mwana wa Saulo alivutwa sana na Daudi, akamupenda kwa moyo wake wote kama alivyojipenda yeye mwenyewe.