Basi, Yakobo akamwambia Simeoni na Lawi: “Ninyi mumeniletea taabu kwa kunifanya nichukiwe na wakaaji wa inchi hii ya Wakanana na Waperizi. Mimi sina watu wengi, na kama wakikusanyika kwa kunishambulia wataniangamiza mimi pamoja na jamaa yangu.”
Siku moja, wakati wa magaribi, Daudi aliamuka toka katika kitanda, akaenda kwenye dari ya nyumba ya kifalme. Alipokuwa anatembea kule juu, alimwona mwanamuke mumoja akioga na mwanamuke yule alikuwa muzuri sana kwa umbo.
Basi, Daudi alituma wajumbe wamulete. Basi Batiseba akakuja kwa Daudi, naye Daudi akalala naye. Kisha akarudi kwake. Mwanamuke yule alikuwa akitoka kujitakasa kisha ugonjwa wake wa mwezi.
Kama kisha hapendezwi naye, atamwacha aende anakotaka. Mwanaume huyo hatamwuzisha kwa kupata feza, wala hatamutendea kama vile mutumwa kwa sababu amemunyenyekeza.
mutawatoa wote wawili inje ya muji na kuwapiga mawe mpaka wakufe. Binti huyo anapaswa kuuawa kwa sababu hakupiga kelele kusudi asaidiwe ingawa alikuwa ndani ya muji; naye mwanaume anapaswa kuuawa kwa sababu amemuchafua muchumba wa mwenzake. Ndivyo mutakavyokomesha uovu huo kati yenu.
mwanaume huyo atamulipa baba wa binti huyo vikoroti makumi tano vya feza kwa sababu amemuchafua, na binti huyo atakuwa muke wake na hatamwacha maisha yake yote.
Gali mwana wa Ebedi, akasema: “Abimeleki ni nani? Sisi hapa Sekemu ni watu wa aina gani hata tumutumikie Abimeleki? Gideoni na Zebuli jemadari wake walimutumikia Hamori baba wa Sekemu, lakini kwa nini basi, sisi tumutumikie Abimeleki?