Rebeka akamwambia Isaka: “Sina raha kabisa katika maisha kwa sababu ya hawa wanawake Wahiti wa Esau. Ikiwa Yakobo ataoa mumoja wa wanawake hawa Wahiti, maisha yangu yana faida gani?”
Hao ndio wana ambao Lea alimuzalia Yakobo kule Padani-Aramu, pamoja na Dina binti yake. Jumla ya wana wake, wabinti zake na wajukuu wake walikuwa watu makumi tatu na watatu.
Na zaidi ya hiyo, wanashikwa na uvivu na kuwa na tabia ya kutangatanga nyumba kwa nyumba. Na si ile tu, vilevile wao ni wakatetea na wenye kujiingiza katika maneno ya watu wengine na kusema maneno yasiyofaa.