Labani aliposikia habari za mwipwa wake Yakobo, alikwenda mbio kumupokea, akamukumbatia, akamubusu, akamukaribisha ndani ya nyumba yake. Yakobo akamwelezea Labani mambo yote yaliyotokea.
sistahili hata kidogo wema wote na uaminifu wote ulionitendea mimi mutumishi wako. Nilipovuka muto Yordani, sikukuwa na kitu isipokuwa fimbo; lakini sasa nina makundi haya mawili.
Yosefu akatoka pahali pale kwa haraka, kwa sababu ya hamu kubwa juu ya ndugu yake, akatafuta pahali pa kulilia. Akaingia ndani ya chumba chake na kuanza kulia.
Chakula kilikuwa kikitwaliwa kutoka kwenye meza ya Yosefu na kupelekwa kwao, lakini Benjamina alipewa mara tano zaidi ya kipimo wandugu zake walichopewa. Basi, wakakunywa na kufurahi pamoja naye.
Yosefu akapanda gari lake la farasi, akakwenda kumupokea baba yake Israeli, kule Goseni. Alipomufikia baba yake, alimukumbatia na kulia kwa kitambo kirefu.
Kwa hiyo Yoabu akaenda na kumwelezea mufalme maneno hayo yote, naye akamwita Abusaloma. Abusaloma akaingia kwa mufalme, akaanguka uso mpaka chini mbele ya mufalme. Na mufalme akamubusu Abusaloma.
Ee Bwana, usikilize maombi yangu mimi mutumishi wako na ya watumishi wako wanaofurahia kukutii wewe. Ninakuomba unifanikishe leo, mimi mutumishi wako, na kunijalia kuhurumiwa na mufalme.” Mimi nilikuwa na madaraka ya kumupa mufalme kinywaji.
Kisha akafunga safari yake na kurudia kwa baba yake. “Alipokuwa angali mbali kidogo, baba yake akamwona, akamusikilia huruma. Akamukimbilia, akamukumbatia mwana wake na kumubusu.
Yule kijana alipokwisha kuondoka, Daudi akasimama na kutoka pahali alipojificha karibu na lundo la mawe. Aliinama chini kwa heshima mara tatu mbele ya Yonatani. Wote wawili, Daudi na Yonatani, wakakumbatiana na kulia. Daudi alikuwa na uchungu zaidi kuliko Yonatani.