Yawe alisimama juu ya ngazi hiyo, akamwambia: “Mimi ni Yawe, Mungu wa Abrahamu baba yako, na Mungu wa Isaka. Nitakupa inchi unayoilalia wewe na wazao wako.
Mimi ndimi yule Mungu aliyekutokea kule Beteli, pahali pale ulipotakasa lile jiwe kwa kulimiminia mafuta na ambapo ulifanyia kiapo. Sasa ondoka katika inchi hii urudi katika inchi yako.’ ”
Nina uwezo wa kukuzuru; lakini Mungu wa baba yako alinitokea usiku wa kuamukia leo, akaniambia nifanye angalisho, akisema: ‘Ujichunge! Usimwambie Yakobo neno lolote, zuri au baya’.
Kama Mungu wa babu yangu Abrahamu, Mungu ambaye ni kitisho cha Isaka, asingelikuwa upande wangu, hakika ungeliniacha niondoke mikono mitupu. Lakini Mungu aliona mateso yangu na kazi niliyofanya kwa mikono yangu, akakukaripia usiku wa kuamukia leo.”
Mungu wa baba yako atakusaidia, Mungu Mwenye Nguvu atakubariki, upate baraka za mvua toka juu mbinguni, baraka za maji ya vilindi vinavyokuwa chini, baraka za uzazi wa wamama na nyama.
Wewe ndiwe Mungu wetu! Uwaazibu, maana sisi hatuna uwezo wowote mbele ya jeshi kubwa kama hili linalotufikia. Hatujui la kufanya lakini tunatazamia musaada kutoka kwako.”
akaomba kwa sauti akisema: “Ee Yawe, Mungu wa babu zetu, wewe ndiwe Mungu unayekuwa mbinguni! Wewe unatawala falme zote katika dunia, una uwezo na nguvu, wala hakuna anayeweza kukupinga.
Kisha Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo.” Musa akafunika uso wake kwa sababu aliogopa kumwangalia Mungu.
Sasa, Daudi alikuwa katika matatizo makubwa kwa sababu watu wake walikuwa na uchungu katika roho zao kwa kupoteza watoto wao. Kwa hiyo wakakuwa wakitaka kumupiga mawe. Lakini Daudi alijipa moyo kwa kumutegemea Yawe, Mungu wake.