Basi, ninakuomba ukubali zawadi niliyokuletea, kwa sababu hata mimi vilevile Mungu amenineemesha, nami nina mali nyingi.” Ndivyo Yakobo alivyomushawishi Esau, naye akapokea zawadi yake.
Esau akasema: “Heri nikuachie sehemu ya watu wangu.” Lakini Yakobo akasema: “Kuna sababu gani ya kufanya hivyo? Inanitosha kwamba mimi nimepata kukubaliwa mbele yako, ewe bwana wangu.”
Halafu Esau akauliza: “Kundi lile nililokutana nalo katika njia lina maana gani?” Yakobo akamujibu: “Nilitumaini kupata kukubaliwa mbele yako, ee bwana wangu.”
Mufalme akamwambia Siba: “Basi, yale yaliyokuwa mali ya Mefiboseti sasa ni mali yako.” Siba akamwambia: “Ninashukuru, bwana wangu mufalme, nami ninaomba nipate kukubaliwa mbele yako siku zote.”
Lakini kama mutumishi yule akijisemesha mwenyewe kwamba bwana wake anakawia kurudia; na halafu anaanza kuwapiga watumishi wenzake, wanaume na wanawake, naye anakula na kunywa na kulewa.
Siku moja, Ruta wa Moabu akamwambia Naomi: “Muniruhusu niende kukusanya masalio ya mavuno pahali nitakapopata kukubaliwa na mwenye shamba.” Naomi akamwambia: “Basi, uende binti yangu.”