Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 32:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Yakobo alituma wajumbe wamutangulie kwenda kwa ndugu yake Esau, kule Seiri, katika inchi ya Edomu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 32:4
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Ee bwana wetu, usikilize; wewe ni kiongozi mukubwa kati yetu. Umuzike marehemu muke wako katika kaburi lolote utakalojichagulia; hakuna yeyote kati yetu atakayekunyima kaburi lake, wala kukuzuia kumuzika marehemu muke wako.”


Kwa hiyo Esau akamwambia Yakobo: “Ninasikia njaa. Tafazali, unigawanyie muchuzi huo mwekundu nikule.” Ndiyo maana walimupanga jina Edomu, maana yake “mwekundu”.


Jamii za watu zikutumikie, na mataifa yainame mbele yako kwa heshima. Ukuwe mutawala wa wandugu zako, na wana wa mama yako wainame mbele yako kwa heshima. Kila mutu anayekulaani alaaniwe, kila mutu anayekubariki abarikiwe!”


Isaka akamujibu: “Nimekwisha kumufanya Yakobo kuwa mutawala wako, na kumupa wandugu zake wote kuwa watumishi wake. Nimemupatia ngano na divai. Nikufanyie nini sasa, wewe mwana wangu?”


Kwa miaka makumi mbili hii yote nimeishi katika nyumba yako. Nilikutumikia miaka kumi na mine kwa ajili ya wabinti zako wawili, na miaka sita nikachunga nyama wako. Lakini wewe, ukabadilisha mushahara wangu mara kumi.


Akamwagiza yule aliyetangulia: “Ndugu yangu Esau atakapokutana nawe na kukuuliza: ‘Wewe ni mutumishi wa nani? Unakwenda wapi? Na nyama hawa ni wa nani?’


Akawapa maagizo haya: “Mutamwambia bwana wangu Esau hivi: Mutumishi wako Yakobo anasema hivi: ‘Nimekaa mugeni kwa Labani mpaka sasa.


Basi, ninakuomba utangulie, nami nitafuata polepole kadiri ya mwendo wa nyama na watoto, mpaka nitakapokufikia kule Seiri.”


Halafu Esau akauliza: “Kundi lile nililokutana nalo katika njia lina maana gani?” Yakobo akamujibu: “Nilitumaini kupata kukubaliwa mbele yako, ee bwana wangu.”


Kwa hiyo, Esau akakwenda kukaa katika inchi ya milima ya Seiri. Jina lingine la Esau ni Edomu.


Hawa ndio wazao wa Esau, baba ya Waedomu katika inchi ya milima ya Seiri.


Ukitenda vyema hautakubaliwa? Na usipotenda vyema, basi, zambi inajificha kwa mulango; inakutamani, lakini unapaswa kuishinda.”


Basi, wakajifungia magunia kwenye viuno na kamba katika shingo yao, wakamwendea mufalme wa Israeli, wakamwambia: “Mutumishi wako, Beni-Hadadi, anakusihi akisema: ‘Tafazali, uniache nipate kuishi.’ ” Ahabu akasema: “Kumbe angali anaishi? Yeye ni ndugu yangu.”


Haruni akamujibu: Ninakuomba, ee bwana wangu, hasira yako isiniwakie mimi mutumishi wako. Unafahamu jinsi watu hawa wanavyokuwa tayari kutenda maovu.


Kujibu kwa upole kunatuliza hasira, lakini neno kali linachochea hasira.


Kwa uvumilivu mutawala anaweza kusadikishwa; ulimi laini unavunja mifupa.


ujue kwamba uko chini ya mamlaka ya mwenzako, lakini mwana wangu, ukitaka kujiokoa, basi fanya hivi: umwendee mutu yule mara moja, umusihi akupe uhuru wako.


Mutawala akikukasirikia, usiache kazi; makosa makubwa yanaweza kufutwa ukiwa munyenyekevu.


Ujumbe wa Mungu juu ya Duma. Ninasikia mutu ananiita kutoka Seiri: Mulinzi, nini kipya leo usiku? Kuna kipya chochote leo usiku?


Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”


Ni vile Sara alimutii Abrahamu, akimwita “Bwana.” Ninyi ni wabinti zake kama mukifanya mema pasipo kuogopa kitisho chochote.


Ee Yawe, ulipotoka kule Seiri, ulipoteremuka kwenye mulima Edomu, inchi ilitetemeka, mbingu zilidondosha maji, mawingu yakaiangusha mvua.


Saulo alitambua sauti ya Daudi, akamwuliza: “Hiyo ni sauti yako mwana wangu Daudi?” Daudi akamujibu: “Bwana wangu mufalme, ni sauti yangu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ