Kwa hiyo Esau akamwambia Yakobo: “Ninasikia njaa. Tafazali, unigawanyie muchuzi huo mwekundu nikule.” Ndiyo maana walimupanga jina Edomu, maana yake “mwekundu”.
Jamii za watu zikutumikie, na mataifa yainame mbele yako kwa heshima. Ukuwe mutawala wa wandugu zako, na wana wa mama yako wainame mbele yako kwa heshima. Kila mutu anayekulaani alaaniwe, kila mutu anayekubariki abarikiwe!”
Isaka akamujibu: “Nimekwisha kumufanya Yakobo kuwa mutawala wako, na kumupa wandugu zake wote kuwa watumishi wake. Nimemupatia ngano na divai. Nikufanyie nini sasa, wewe mwana wangu?”
Kwa miaka makumi mbili hii yote nimeishi katika nyumba yako. Nilikutumikia miaka kumi na mine kwa ajili ya wabinti zako wawili, na miaka sita nikachunga nyama wako. Lakini wewe, ukabadilisha mushahara wangu mara kumi.
Akamwagiza yule aliyetangulia: “Ndugu yangu Esau atakapokutana nawe na kukuuliza: ‘Wewe ni mutumishi wa nani? Unakwenda wapi? Na nyama hawa ni wa nani?’
Halafu Esau akauliza: “Kundi lile nililokutana nalo katika njia lina maana gani?” Yakobo akamujibu: “Nilitumaini kupata kukubaliwa mbele yako, ee bwana wangu.”
ujue kwamba uko chini ya mamlaka ya mwenzako, lakini mwana wangu, ukitaka kujiokoa, basi fanya hivi: umwendee mutu yule mara moja, umusihi akupe uhuru wako.