Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 32:31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

31 Yakobo akaita pahali pale Penueli, akisema: “Nimemwona Mungu uso kwa uso, nami sikukufa.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 32:31
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Hagari akamupa Yawe aliyezungumuza naye kule jina la “Wewe ni Mungu Anayeona,” kwa maana alifikiri: “Kweli hapa nimemwona yeye anayeniona?”


Kulipokucha, wamalaika wakamusihi Loti wakisema: “Amuka, utwae muke wako na hawa wabinti zako wawili musipate kuangamia wakati muji huu unapoazibiwa.”


Jua lilikuwa limekwisha kupanda juu wakati Loti alipofika katika muji wa Soari.


Yakobo akabaki peke yake. Kisha mutu mumoja akakuja, akapigana naye mpaka asubui.


Jua lilikuwa limekwisha kupanda wakati Yakobo alipoondoka Penueli, akakuwa anachechemea kwa sababu ya kiuno chake.


Nyuma ya mambo hayo, mufalme Yeroboamu akaujenga upya muji wa Sekemu kwenye mulima wa Efuraimu. Akakaa kule. Kisha akaenda kujenga muji wa Penueli.


Hao manabii wakamutwaa ngombe dume wao waliyepewa, wakamutayarisha, kisha wakaanza kumulilia Bali kutokea asubui mpaka saa sita za muchana, wakirukaruka pembeni ya mazabahu waliyotengeneza wakisema: “Ee Bali, utusikilize!” Lakini hakukutokea sauti yoyote, wala hakuna aliyewajibu.


Ninakuomba tu waadui wasinisimange, wasijitukuze juu ya kuanguka kwangu.


wakamwona Mungu wa Israeli. Chini ya miguu yake kulikuwa kitu kama sakafu ya mawe ya yakuti samawi, kikiwa safi kama mbingu inayoangaa.


Na Mungu hakuwazuru wale viongozi wa watu wa Israeli. Walimwona Mungu, wakakula na kunywa.


Basi, mimi nikasema: Ole kwangu! Mimi nimeangamia, maana, midomo yangu ni michafu, na watu ninaoishi nao ni wenye midomo michafu. Hata hivyo, kwa macho yangu mwenyewe, nimemwona Mufalme, Yawe wa majeshi.


Lakini, kusudi nisijivune kupita kipimo kwa ajili ya kupokea ufunuo wa ajabu, nilitiwa katika mwili wangu kitu kinachoniumiza kama mwiba. Kitu kile ni kama mujumbe wa Shetani kwa kunipiga na kunizuiza nisijivune kupita kipimo.


Lakini akanijibu: “Neema yangu inakutoshelea, kwa maana uwezo wangu unatimizwa katika uzaifu.” Basi tafazali nijivunie sana uzaifu wangu kusudi nijazwe na uwezo wa Kristo.


wakasema: ‘Sikiliza! Yawe, Mungu wetu, ametufunulia utukufu na ukubwa wake. Tumeisikia sauti yake kutoka katikati ya ule moto. Leo hivi tumemwona Mungu akisema na mwanadamu, naye mwanadamu pahali pa kufa akaendelea kuishi!


Ni mwanadamu gani aliyepata kusikia sauti ya Mungu Mwenye Uzima kutoka katikati ya moto kama vile tulivyomusikia sisi halafu akaweza kubaki muzima?


Halafu Gideoni akatambua kwamba huyo alikuwa malaika wa Yawe; akasema: “Ole wangu, ee Bwana wangu Yawe, maana nimemwona malaika wako uso kwa uso.”


Lakini Yawe akamwambia: “Amani ikuwe nawe! Usiogope, hautakufa.”


Kutoka kule akawaendea watu wa Penueli, akawaomba namna ileile. Nao watu wa Penueli wakamujibu kama vile watu wa Sukoti walivyomujibu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ