Alitwaa mawe kumi na mawili, hesabu ya makabila kumi na mawili yaliyopewa majina ya wana wa Yakobo ambaye neno la Yawe lilimufikia kusema hivi: “Jina lako litakuwa Israeli.”
Hata sasa wanatenda kama vile walivyofanya zamani. Hawamwabudu Yawe, wala hawafuati masharti, maagizo, sheria au amri ambazo yeye Yawe aliwaamuru wana wa Yakobo; ambaye alimupa jina la Israeli.
Yawe aliyewaumba enyi watu wa Yakobo, yeye aliyewafanya enyi watu wa Israeli, anasema hivi: Musiogope, maana mimi nimewakomboa; nimewaita kwa jina lenu nanyi ni wangu.
Kisha akamupeleka Simoni kwa Yesu. Yesu akamwangalia, akasema: “Wewe ndiwe Simoni mwana wa Yoane, sasa utaitwa Kefa.” (Jina “Kefa” ni sawasawa na “Petro” na maana yake ni “Jiwe.”)
“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda, nitamupa ile mana iliyofichwa. Na nitamupa vilevile jiwe dogo jeupe, na juu yake kumeandikwa jina jipya ambalo hakuna mutu yeyote anayelijua, isipokuwa tu yule anayelipewa.