Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 32:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Mutu yule alipoona kwamba hawezi kumushinda Yakobo, alimugusa Yakobo kwenye maunganio ya kiuno, naye akateguka alipokuwa anapigana naye.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 32:26
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yakobo akabaki peke yake. Kisha mutu mumoja akakuja, akapigana naye mpaka asubui.


Kisha yule mutu akamwambia Yakobo: “Uniache nijiendee, maana kunapambazuka.” Lakini Yakobo akamwambia: “Sitakuacha hata kidogo, mpaka umenibariki!”


Lakini Yebesi alimwomba Mungu wa Israeli akisema: “Ee Mungu, ninakusihi unibariki na kupanua mipaka yangu. Mukono wako ukuwe pamoja nami na unilinde kutokana na jambo lolote ovu, na mateso yasinipate.” Naye Mungu akamupa yale aliyoomba.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa vyombo vyenye nyuzi. Zaburi. Wimbo.


Sasa, usijaribu kunizuia. Uniache niwaangamize kwa kasirani kali. Kisha kutokana nawe nitaunda taifa kubwa.


Mara tu nilipoachana nao, nikamwona mupenzi wangu wa moyo. Nikamushika wala sikumwacha aondoke, mpaka nilipomupeleka katika nyumba kwa mama yangu, mpaka ndani ya chumba cha yule aliyenizaa.


Shingo yako ni kama munara wa pembe za tembo. Macho yako ni kama visima vya muji wa Hesiboni, karibu na mulango wa Beti-Rabi. Pua yako ni kama munara wa Lebanoni, ambao unauelekea muji wa Damasiki.


Yawe, Mutakatifu wa Israeli, Mungu, Muumba wa Israeli anasema hivi: Munataka kuniuliza juu ya watoto wangu, au kuniamuru juu ya kazi zangu mwenyewe?


Hata hivyo, ee Yawe, wewe ni Baba yetu. Sisi ni kama udongo, wewe ni mufinyanzi. Sisi wote ni kazi ya mikono yako.


Yakobo akiwa angali katika tumbo la mama yake, alimushika kaka yake kisigino. Na alipokuwa mutu muzima alishindana na Mungu.


Lakini katika mambo haya yote tunapata ushindi kabisa kwa njia ya yule aliyetupenda.


Basi wandugu zangu wapenzi, musimame imara bila kutikisika. Muendelee kumutumikia Bwana siku zote, mukijua kwamba masumbuko munayopata kwa ajili ya Bwana hayatapita bure.


Uniache niwaangamize, nifute jina lao toka katika dunia. Nami nitakufanya wewe kuwa taifa lenye nguvu na kubwa kuliko wao.’


Wakati Yesu alipoishi katika dunia, aliomba na kusihi kwa malalamiko makubwa pamoja na kutoa machozi kwa Mungu ambaye angeweza kumwokoa toka katika kifo. Mungu alimusikia Yesu kwa sababu yeye alimuheshimu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ