Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 32:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Akatoa agizo hilohilo kwa mutumishi wa kundi la pili na la tatu na wengine wote, akisema: “Mutamwambia Esau maneno hayohayo mutakapokutana naye.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 32:20
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wewe utamujibu: ‘Hii ni mali ya mutumishi wako Yakobo, nayo ni zawadi yako wewe bwana wangu Esau. Tena Yakobo mwenyewe yuko nyuma anafuata.’ ”


Zaidi ya yote, mutamwambia: ‘Mutumishi wako Yakobo yuko nyuma, anafuata.’ ” Yakobo alifanya hivyo akifikiri: “Pengine nitamutuliza kwa zawadi hizi ninazomutangulizia na kisha nitaweza kuonana naye macho kwa macho; labda atanipokea.”


Hapo Israeli, baba yao, akawaambia: “Basi! Kwa vile ni lazima ikuwe hivyo basi, mufanye hivi: mutwae katika mifuko yenu sehemu ya mazao bora ya inchi yetu, mumupelekee zawadi yule mukubwa. Mumupelekee mafuta kidogo ya mukwaju, asali kidogo, ubani, marasi, kungu na lozi.


Watumishi wake wakamwendea, wakamwambia: “Tumesikia kwamba wafalme wa Israeli ni wema. Basi, uturuhusu tujifunge magunia kwenye viuno na kamba katika shingo, tumwendee mufalme wa Israeli. Labda atayaokoa maisha yako.”


Mutu wa hasira mbaya anasababisha ugomvi, lakini asiyekuwa mwepesi wa hasira anautuliza.


Hasira ya mufalme ni kama mujumbe wa kifo; mutu mwenye hekima ataituliza.


Zawadi inamufungulia mutu milango; inaweza kumufikisha mutu mbele ya mukubwa.


Hasira inatulizwa kwa zawadi ya siri; kituliro kinachotolewa kwa uficho kinatuliza kasirani.


Hatakubali malipo yoyote; wala kutulizwa na zawadi zako nyingi.


Labda Mungu atabadilisha nia yake, na kuacha kutukasirikia, nasi hatutaangamizwa!


Anapaswa kuwaonya kwa upole wale wanaopingana naye; kwa maana labda Mungu anaweza kuwajalia hata wapate kugeuka toka zambi na kutambua ukweli.


Basi mufanye sanamu zenu za majipu na sanamu za panya, vitu ambavyo vinaangamiza inchi yenu, nanyi mutamutukuza Mungu wa Israeli. Labda ataacha kuwaazibu ninyi wenyewe, miungu yenu na inchi yenu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ