Zaidi ya yote, mutamwambia: ‘Mutumishi wako Yakobo yuko nyuma, anafuata.’ ” Yakobo alifanya hivyo akifikiri: “Pengine nitamutuliza kwa zawadi hizi ninazomutangulizia na kisha nitaweza kuonana naye macho kwa macho; labda atanipokea.”
Hapo Israeli, baba yao, akawaambia: “Basi! Kwa vile ni lazima ikuwe hivyo basi, mufanye hivi: mutwae katika mifuko yenu sehemu ya mazao bora ya inchi yetu, mumupelekee zawadi yule mukubwa. Mumupelekee mafuta kidogo ya mukwaju, asali kidogo, ubani, marasi, kungu na lozi.
Watumishi wake wakamwendea, wakamwambia: “Tumesikia kwamba wafalme wa Israeli ni wema. Basi, uturuhusu tujifunge magunia kwenye viuno na kamba katika shingo, tumwendee mufalme wa Israeli. Labda atayaokoa maisha yako.”
Basi mufanye sanamu zenu za majipu na sanamu za panya, vitu ambavyo vinaangamiza inchi yenu, nanyi mutamutukuza Mungu wa Israeli. Labda ataacha kuwaazibu ninyi wenyewe, miungu yenu na inchi yenu.