16 ngamia makumi tatu wanaonyonyesha pamoja na watoto wao, ngombe dike makumi ine, ngombe dume kumi, punda dike makumi mbili, na dume kumi.
mbuzi dike mia mbili na mabeberu makumi mbili, kondoo dike mia mbili, na dume makumi mbili,
Akawapatia watumishi wake, kila mumoja kundi lake, akawaambia: “Mutangulie mukiacha nafasi kati ya kundi na kundi katika mustari wenu.”
Akatoa agizo hilohilo kwa mutumishi wa kundi la pili na la tatu na wengine wote, akisema: “Mutamwambia Esau maneno hayohayo mutakapokutana naye.
Mutu muzuri anakopesha bila faida; anafanya shuguli zake kwa kutumia haki.
Hekima itakulinda, ufahamu utakuchunga;
Mutu huyo anajua kufanya vile, kwa sababu Mungu wake anamufundisha.
“Muangalie! Ninawatuma kama kondoo katikati ya imbwa wa pori. Basi mukuwe waangalifu kama nyoka na wakamilifu kama njiwa.
Akamwambia yule kijana wake: “Utangulie! Mimi nitakufuata.” Lakini hakumwambia mume wake neno lolote.