Uwakumbuke watumishi wako, Abrahamu, Isaka na Israeli, ambao uliwaapia kwa nafsi yako mwenyewe, ukisema: Nitawazidisha wazao wenu kama nyota za mbinguni na inchi yote hii niliyowaahidia nitawapa vizazi vyenu wairizi milele.
Kwa sababu hiyo, kwa njia ya mutu mumoja aliyekuwa akingojea kufa, kukazaliwa wazao wengi sana kama nyota na kama muchanga unaokuwa kandokando ya bahari.
Naye Mungu, kwa sababu alitaka kuonyesha wazi kwa wale watakaopokea ahadi kwamba yeye hawezi kubadilisha shauri lake hata kidogo, akaihakikisha kwa kiapo.