Usiku uleule Yawe alimutokea na kumwambia: “Mimi ni Mungu wa baba yako Abrahamu. Usiogope; niko pamoja nawe. Nitakubariki na kuwazidisha wazao wako kwa ajili ya Abrahamu, mutumishi wangu.”
Yawe alisimama juu ya ngazi hiyo, akamwambia: “Mimi ni Yawe, Mungu wa Abrahamu baba yako, na Mungu wa Isaka. Nitakupa inchi unayoilalia wewe na wazao wako.
Mimi ndimi yule Mungu aliyekutokea kule Beteli, pahali pale ulipotakasa lile jiwe kwa kulimiminia mafuta na ambapo ulifanyia kiapo. Sasa ondoka katika inchi hii urudi katika inchi yako.’ ”
Nina uwezo wa kukuzuru; lakini Mungu wa baba yako alinitokea usiku wa kuamukia leo, akaniambia nifanye angalisho, akisema: ‘Ujichunge! Usimwambie Yakobo neno lolote, zuri au baya’.
Kama Mungu wa babu yangu Abrahamu, Mungu ambaye ni kitisho cha Isaka, asingelikuwa upande wangu, hakika ungeliniacha niondoke mikono mitupu. Lakini Mungu aliona mateso yangu na kazi niliyofanya kwa mikono yangu, akakukaripia usiku wa kuamukia leo.”
Kisha Israeli akamubariki Yosefu, akisema: “Mungu ambaye babu zangu Abrahamu na Isaka walimutii katika maisha yao, Mungu ambaye ameniongoza katika maisha yangu mpaka leo,
‘Mumwambie Yosefu kwa ajili yangu: Tafazali uwasamehe wandugu zako makosa yao mabaya na maovu yote waliyokutendea.’ Sasa basi, tafazali usamehe uovu tuliokutendea sisi watumishi wa Mungu wa baba yako.” Yosefu alipopata ujumbe huu, akalia.
Musijiachilie kutawaliwa na tamaa ya mali katika maisha yenu, lakini mutoshelewe na vitu munavyokuwa navyo, kwa maana Mungu mwenyewe amesema: “Sitakusahau wala kukuachilia.”