7 Biliha, mujakazi wa Rakeli, akapata mimba tena na kumuzalia Yakobo mutoto wa pili mwanaume.
Rakeli akasema: “Mungu amenitendea sawa, amesikia kilio changu na kunipa mutoto mwanaume.” Akamwita mutoto yule Dani.
Halafu Rakeli akasema: “Nimepigana mapigano makubwa na dada yangu, nami nimeshinda.” Kwa hiyo akamwita mutoto yule Nafutali.
Nafutali na wana wake: Yaseli, Guni, Yeseri na Silemu.
Hao saba ni wazao wa Yakobo na Biliha, mujakazi ambaye Labani alimupa binti yake Rakeli.
Kabila la Nafutali, litapata eneo linalopakana na lile la Aseri, kutoka mashariki mpaka magaribi.