Hivyo, siku zinazokuja, uaminifu wangu utaonekana waziwazi utakapokuja kuangalia mushahara wangu. Mbuzi yeyote asiyekuwa na madoadoa au matakamataka, au kondoo yeyote asiyekuwa mweusi akionekana katika kundi langu, yule atakuwa ameibiwa.”
Lakini siku hiyohiyo Labani akakwenda akatenga beberu wote wenye mistari na madoadoa, mbuzi wote dike waliokuwa na madoadoa na matakamataka, kila nyama aliyekuwa na weupe kwenye mwili wake, na kila kondoo mweusi, akawaweka chini ya ulinzi wa wana wake.
Ninataka ninyi wote museme kwa luga za ajabu, lakini ninataka zaidi tena mupate kutabiri. Kwa maana, yule anayetabiri ni wa lazima kuliko yule anayesema kwa luga za ajabu, isipokuwa kama huyo mutu anaweza kutafsiri yale anayosema kusudi kanisa zima lijengwe katika imani.